Katika
nchi ya Namibia kuna mambo mengi mazuri ya kuifanya nchi hiyo itembelewe na
watu mbali mbali hasa kwenye swala la kuenzi na kuziendeleza tamaduni zao.
Ovahimba
na Ovazimba kutoka pande za Kunene na Omusati wamekua wakiziendeleza tamaduni
zao hasa kwenye kupokea wageni.
Katika
jamii hiyo wageni wakiume
wanapowatembelea wanapewa walale na mke wa mmoja wa mwanafamilia, endapo kura
za wengi zitaangukia kwake.
Mume
huyo atapaswa aondoke chumba wanacholala na mke wake ili ampishe mgeni na
kuhamia chumba kingine.
Iwapo
wanakaa nyumba yenye chumba kimoja
itabidi mwanaume akatafute sehemu
nyingine akalale.
Mwanamke
katika jamii hiyo anaweza kuwa na maamuzi madogo au kutokuwa na maamuzi kabisa,
na endapo anarafiki zake inamlazimu awape kwa mume wake, japo haifanyiki mara
nyingi.
0 comments:
Post a Comment