Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa,
ametangaza baraza lake jipya la mawaziri.
Waziri wa zamani wa fedha Nhlanhla Nene amerejeshwa tena
katika nafasi hiyo.
Nene alifukuzwa Disemba 2015 na Rais wa zamani
Jacob Zuma na nafasi yake ikachukuliwa na Des van Rooyen.
Palipotokea anguko la thamani ya randi
alilazimika kumfukuza Rooyen na kumchagua Pravin Gordhan, siku nne baadae
ambaye pia alimfukuza kazi siku za mbeleni.
Katika baraza la Ramaphosa Gordhan amerejea
kama waziri wa masuala la biashara.
Aliyekuwa mke wake Zuma Nkosazana Dlamini-Zuma,
ameteuliwa kuwa waziri wa ofisi wa rais.
Bw Ramaphosa ambaye ni mfanya biashara wa umri
wa miaka 65, katika hotuba yake ya taifa awali mwezi huu, aliahidi kupambana na
rushwa na kuboresha uchumi wa nchi hio.
0 comments:
Post a Comment