This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Monday 17 December 2012

Fahamu Siri ya herufi ya mwanzo ya Jina lako...

Je Unajua Siri ya herufi ya mwanzo ya jina lako?. Soma hapa utaweza kuelewa Tabia zako au tabia za rafiki au mpenzi wako. >HERUFI A >Mwenye jina linaloanziana na herufi A ni mtu anayependa mambo makubwa, anajiamini na mwenye uwezo wa kutimiza malengo yake. Ni mtu mwenye tahadhari, mchangamfu na mpenda matukio. Anapenda Kuheshimiwa, anapenda Mamlaka, na ana kiburi, na hasira. Herufi A inawakilisha Nyota ya Punda. >HERUFI B >Mwenye jina linaloanziana na herufi B ni mtu, mkarimu, muaminifu, na hupenda kazi. Ni Jasiri, shujaa na mkatili katika vita au pale anapotaka kulinda vilivyo katika himaya yake. Herufi B inawakilisha Nyota ya Ngombe, >HERUFI C >Mwenye jina linaloanziana na herufi C ni mtu wa kukubadilika badilika, mshindani na hupenda kupigania malengo yao wanayopenda. Ni watu wa wabunifu na wanaopenda mawasiliano Herufi C inawakilisha Nyota ya Mapacha, >HERUFI D >Mwenye jina linaloanziana na herufi D ni mtu anayependa usawa, Biashara. Ni watu wanaopenda kuamrisha na mwenye kupenda usafi. Ni jeuri na wenye msimamo. Herufi C inawakilisha Nyota ya Kaa, >HERUFI E >Mwenye jina linaloanzia na herufi E ni mtu mwenye roho nzuri ,yenye mapenzi na huruma. mwenye kupenda uhuru katika mapenzi na mchangamfu. Kinyume na hivyo atakuwa ni mtu asiotegemewa na kigeugeu. Herufi E inawakilisha Nyota ya Simba, > >HERUFI F >Mwenye jina linaloanzia na herufi F ni mtu mwenye mapenzi,huruma , roho nzuri na ana uwezo wa kuwafariji watu. Ni mtetezi wa watu na mwenye huzuni lakini ni mzito wa kufanya maamuzi. Herufi F inawakilisha Nyota ya Mashuke, >HERUFI G >Mwenye jina linaloanzia na herufi G ni mtu mwenye mwenye imani ya kidini na nguvu za kiroho. Ana kipaji cha kubuni na uwezo wa kutatua matatizo ya watu. ni mtu mwenye hisia kali,msomi, mpweke na mkaidi wa kukubali ushauri wa kutoka kwa watu. Herufi G inawakilisha Nyota ya Mizani, >HERUFI H >Mwenye jina linaloanzia na herufi H ni mtu mwenye ubunifu na nguvu katika biashara, hupata faida kubwa kutokana na jitihada na bidii zake. ni mwenye mawazo mengi, mchoyo na mbinafsi. Herufi H inawakilisha Nyota ya Nge, >HERUFI I >Mwenye jina linaloanzia na herufi I ni mtu mwenye kupenda sheria, ana huruma na utu. Wakati mwingi hajiamini na ni mwenye hasira za haraka. Herufi I inawakilisha Nyota ya Mshale, >HERUFI J >Mwenye jina linaloanzia na herufi J ni mtu mwenye matamanio,mkweli, mkarimu na muerevu. asiyekubali kushindwa na hupata mafanikio makubwa. Wakati mwingine anakuwa ni mtu mvivu na aliyekosa mwelekeo. Herufi J inawakilisha Nyota ya Mbuzi, >HERUFI K >Mwenye jina linaloanzia na herufi K ni mtu mwenye jeuri. mwenye msimamo thabiti,mashuhuri na mwenye uwezo wa kushawishi na kuamsha hisia za watu wana uwezo wa utambuzi ambao watu wengi hawana. ni mtu asioridhika na hali ya kimaisha. Herufi K inawakilisha Nyota ya Ndoo, >HERUFI L >Mwenye jina linaloanzia na herufi L ni mtu wa vitendo, mwenye hisani na aliyejipanga vizuri kimaisha. Huwa wanapata ajali mara kwa mara. Herufi L inawakilisha Nyota ya Samaki, >HERUFI M >Mwenye jina linaloanzia na herufi M ni mtu mwenye kujiamini sana, mchapakazi na hupata mafanikio. ni mtu mropokaji,mwenye haraka na mwepesi kukasirika. Herufi M inawakilisha Nyota ya Punda >HERUFI N >Mwenye jina linaloanzia na herufi N ni mtu mwenye ubunifu, hisia kali na hupenda kuwasiliana lakini ana wivu sana. Herufi N inawakilisha Nyota ya Ngombe > >HERUFI O >Mwenye jina linaloanzia na herufi O ni mtu mwenye subra, mvumilivu na mwenye bidii ya kusoma. Ni mtu mwenye kupenda kutumikia jamii na mwenye uwezo mkubwa wa kudhibiti hisia. Herufi O inawakilisha Nyota ya Mapacha >HERUFI P >Mwenye jina linaloanzia na herufi P ni mtu mwenye uwezo wa kuamrisha na hekima kubwa. Ana nguvu za kiroho lakini anapenda sana kujitumbukiza kwenye mambo ya watu. Herufi P inawakilisha Nyota ya Kaa >HERUFI Q >Mwenye jina linaloanzia na herufi Q ni mtu mwenye kupenda mambo ya asili. Ni watu wasiyoelezeka nawana uwezo wa kuonyesha vitu visivyojulikana hata hivyo ni mtu aliyepooza sana. Herufi Q inawakilisha Nyota ya Simba >HERUFI R >Mwenye jina linaloanzia na herufi R ni mtu mwenye uvumilivu, wenye huruma lakini ana hasira za haraka. Muda wote anakuwa mpenda amani. Herufi R inawakilisha Nyota ya Mashuke >HERUFI S >Mwenye jina linaloanzia na herufi S ni mtu mwenye mvuto mkali wa kuleta utajiri. Ni watu wenye maamuzi ya ghafla na hupenda mageuzi makubwa. Herufi S inawakilisha Nyota ya Mizani >HERUFI T >Mwenye jina linaloanzia na herufi T ni mtu mwenye kupenda ushauri wa kiroho, anatumia nguvu za ziada kusaidia watu na hupata mafanikio baada ya muda mrefu. Ni watu wenye hisia kali sana na ni wepesi kushawishika. Herufi S inawakilisha Nyota ya Nge >HERUFI U >Mwenye jina linaloanzia na herufi U ni mtu mwenye bahati kubwa kwa ujumla. Anapenda uhuru katika mapenzi. Lakini ni mtu mbinafsi, mwenye tamaa na aliyekosa maamuzi. Herufi U inawakilisha Nyota ya Mshale. >HERUFI V >Mwenye jina linaloanzia na herufi V ni mtu Mchapakazi, wenye bidii na asie choka. Hata hivyo ni watu wasiotabirika. Herufi U inawakilisha Nyota ya Mbuzi. >HERUFI W >Mwenye jina linaloanzia na herufi W ni mtu muwazi, wachangamfuu kupita kiasi na mwenye uwezo wa kutambua mtu mwema na mbaya. Ni watu wenye tamaa na hufanya mambo ya hatari. Herufi W inawakilisha Nyota ya Ndoo. >HERUFI X >Mwenye jina linaloanzia na herufi X ni mtu asiyependa kuwekewa vizuizi katika kwenye anasa na ni rahisi kujiingiza kwenye uzinzi na kujitoa uaminifu. Herufi X inawakilisha Nyota ya Samaki. >HERUFI Y (YASINTA) >Mwenye jina linaloanzia na herufi Y ni mtu mwenye kupenda Uhuru na hawapendi kupingwa jambo lao lolote. Ni watu wanaokosa uamuzi na husababishia kupoteza bahati katika maisha. Herufi Y inawakilisha Nyota ya Punda >HERUFI Z >Mwenye jina linaloanzia na herufi Z ni mtu mwenye kupenda matumaini na amani. Ni wenye msimamo mkali ila wanashauriwa kufikiria kabla ya kuamua jambo. Herufi Z inawakilisha Nyota ya Ngombe.

Wednesday 12 December 2012

UNAJUA KUWA SHULE YA KWANZA TANZANIA ILIJENGWA MUHEZA TANGA?

HAYA NI BAADHI YA MAJENGO YALIYOJENGWA KATIKA SHULE HIYO BAADAE.... MWAKA 1848 Mmishenari wa Kijerumani Dk Johan Ludwig Krapf,alitembelea kijiji cha Magila kilichopo Muheza mkoani Tanga akiwa katika safari zake za Afrika Mashariki. Magila kuna mlima ulio katika safu za milima ya Usambara ukipakana na mlima wa Magoroto ambao ndio chanzo cha maji ya mto Mkurumuzi unaoelekea Muheza. Historia inaonyesha eneo la mlima Magila wenye miamba na mawe mengi, zamani kabla ya kuja wageni lilitumika kuwatenga wagonjwa wa ukoma na magonjwa mengine yasiyotibika, kwa lengo la kuwazuia wasiwaambukize wengine. Dk Krapf alipofika na kuwaona wagonjwa hao waliokuwa wakiishi kwa madhila makubwa, alichonga msalaba katika mti wa mkuyu kwa imani kuwa Mwenyezi Mungu angewaponya wagonjwa hao. Eneo hilo ndilo lililokuja kujengwa shule ya kwanza na Waingereza mwaka 1886. Alama ya msalaba huo ipo hadi na sasa na ndipo ilipo Shule ya Sekondari Hegongo. Hadi leo mahali hapo panaitwa Magila Msalabani. Kwa sasa Magila ni kata yenye vijiji vya vya Magila, Mikwamba, Misongeni na Mafleta. Mkaazi wa eneo hilo Luteni Kanali mstaafu John Mhina amekamilisha kuandika kitabu kuhusu historia ya Magila Msalabani,kinachoeleza historia ya kijiji hicho na ujio wa wazungu walioanzisha shule ya kwanza Tanganyika na kanisa. Luteni Kanali Mhina aliyelitumikia Taifa kwa muda mrefu kama mwanajeshi, na baadaye kuwa Mbunge wa Muheza kutoka mwaka 1990 hadi 1995,anasema harakati za kuanzisha shule katika kijiji hicho zilitokana na Wamishenari waliokuja Afrika Mashariki kutoka Ulaya kwaajili ya kueneza dini ya kikristo tangu miaka ya 1770. Anawataja baadhi ya Wamishenari hao kuwa ni pamoja na David Livingstone,Charles Mackenzie, William Tozer na Edward Steer. Anasema harakati hizo zilianzia tangu visiwa vya Zanzibar mwaka 1863 ambako pia walikomesha biashara ya utumwa na kuanza ujenzi wa kanisa la Anglikana la Mkunazini Zanzibar kwa miaka 10 tangu mwaka 1873. Anasema wakati huo kulikuwa na shule iliyoanzishwa Zanzibar maeneo ya Kiungani na Kiinua mguu na Askofu William Tozer mwaka 1869. Hata hivyo, anasema shule hiyo haikuwa rasmi na ilikuwa ikifundisha elimu ya dini kwa watumwa waliokombolewa.

Wednesday 21 November 2012

HILI LINAWAHUSU WANAWAKE ZAIDIII SOMA…

Jee unajua kuwa kufanya kazi usiku ni hatari kwa akina mama? Na inaweza kusababisha kifo? Utafiti uliofanywa na madaktari nchini Uingereza umegundua kuwa wanawake wanaopendelea kufanya kazi usiku wanahatari ya kupatikana na sartani ya matiti-breast cancer. Katika kichwa cha Kazi za usiku zinasababisha vifo 500 kila mwaka nchini Uingereza utafiti hunasema shift za usiku ni hatari kwa akina amma. Dr Lesley Rushton,wa Imperial College Mjini London anasema Mawanamke akifanya kazi ya usiku kwa wastani ya siku tatu kwa wiki kwa miaka sita - anakaribisha kansa ya matiti. Kufanya kazi usiku au kukosa usingizi kwa akina mama kunatatiza utengenezaji wa homoni ya ya MELATONI, hii ni chembechembe inayosaidia usingizi na hii inasadikiwa kuwa na uwezo wa zuia kansa.

Tambua Madhara ya Sindano za uzazi wa mpango....

UTAFITI umebaini kuwa sindano za uzazi wa mpango zinachangia kasi ya maambukizi ya virusi vya Ukimwi,kwa kuwa zina vichocheo vingi ambavyo vinahuisha virusi vya Ukimwi katika nyumba ya uzazi na kuvipa nguvu ya kusambaa. Inaelezwa kuwa walio katika hatari zaidi ya maambukizi hayo ni wanawake walioko katika ndoa kwa kuwa ndiyo wanaotumia zaidi sindano hizo. Utafiti huo uliofanywa na wanasayansi wa Marekani na kuripotiwa na gazeti la The Guardian la Uingereza, umebaini kuwa wanawake wanaotumia sindano za uzazi wa mpango wapo katika hatari mara mbili ya kupata maambukizi ya Ukimwi au kuwaambukiza wenzi wao, kuliko wengine. Katika utafiti huo uliofanywa katika nchi saba zinazoendelea barani Afrika ikiwamo Tanzania, wanasayansi hao kutoka Chuo Kikuu cha Washington,walipendekeza ushauri zaidi utolewe kwa wanandoa kabla mtu hajajiingiza kwenye matumizi ya sindano kama njia ya kupanga uzazi. Utafiti huo ulifanyika kwa wanandoa 3,790 kutoka nchi za Tanzania, Afrika Kusini, Zimbabwe, Uganda, Kenya, Rwanda na Botswana, ulichapishwa kwa mara ya kwanza katika Jarida la Afya la Lancet kabla ya kunukuliwa na gazeti la The Guardian. Utafiti umebaini pia kuwa zaidi ya wanawake 140 milioni duniani,wanatumia njia mbalimbali za uzazi wa mpango, huku wanandoa wengi katika nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara, wanaoishi na VVU wakichagua kutumia sindano kama njia ya kuzuia mimba zisizotarajiwa. Wanasayansi hao walikusanya taarifa kati ya wanandoa 3,790 ambao mmoja wao anaishi na VVU na mwenza wake akiwa hana maambukizo. Aidha wanawake ambao wanaishi na VVU na wanatumia sindano hizo pia,walikuwa katika hatari zaidi ya kuwaambukiza wenzi wao. Vipimo vilionyesha kuwa sindano hizo ambazo zina vichocheo ambavyo vinavipa nguvu virusi ndani ya nyumba ya uzazi (cervix). Imeelezwa kuwa njia za uzazi wa mpango zinazohamasishwa zaidi na kupendwa zaidi na wanawake ni sindano, ambazo wanawake wanasema kuwa zinadumu kwa muda mrefu na zinaweza kutumika bila ya ruhusa au mume kufahamu. Kiongozi mkuu wa utafiti huo Renee Heffron wa Chuo Kikuu cha Washington,alisema sindano za uzazi wa mpango zina vichocheo vingi ambavyo huvihuisha vijidudu vya Ukimwi katika nyumba ya uzazi na kuvipa nguvu ya kusambaa. Mwanasayansi mwingine, Charles Morrison wa Kituo cha Afya cha Durham, nchini Marekani alisema uhamasishaji wa matumizi ya sindano za uzazi wa mpango unachochea maambukizi zaidi katika nchi za Jangwa la Sahara. Na ameshauri nchi zinazoendelea kuacha matumizi ya njia za uzazi wa mpango zenye vichocheo, ili tupunguze maambukizi. Alivitaka vituo vya afya vitoe ushauri kwa wanawake kutumia kondomu badala ya sindano au vidonge. Mara nyingi watu wanaotumia vidonge, wengi si wanandoa, mtu anayemeza vidonge vya kuzuia mimba anaogopa zaidi mimba si Ukimwi. Huchoche hamu ya mapenzi. Mfamasia katika Kitengo cha Dawa kwa watu wanaoishina VVU katika Hospitali ya Amana Christopher Masika,alisema anaafiki kuwa sindano na hata vidonge vinaweza kuwa ni sababu inayochochea maambukizi kwa sababu ya uhuru. Kwa sababau Mtu anapotumia sindano huwa huru kufanya ngono,kwa kuwa hana hofu ya mimba hicho kinaweza kumfanya apate maambukizi kwa urahisi, tofauti na anapotumia kondomu. Amesema wapo baadhi ambao wakitumia sindano hizo vichocheo vinawafanya wapate hamu zaidi ya kufanya mapenzi, hivyo huanza kutembea na wanaume wengine.

Monday 5 November 2012

VYAKULA TUNAVYOKULA VINAVYOTUMALIZAAaaaa

Tukumbuke kwamba uzima wa mtu unategemea sana kinga aliyonayo mwilini,kinga ambayo hujengwa na ulaji wa vyakula vyenye virutubisho vya aina mbalimbali. Kwa namna ambavyo Mungu ametuumba, mwili unapaswa kujilindi wenyewe dhidi ya maradhi ya kila aina. Ukiwa na kinga imara ya mwili siyo rahisi kuugua mara kwa mara. Magonjwa yanayojitokeza haraka pale kinga ya mwili inapokuwa chini, ni pamoja na kuugua malaria mara kwa mara, kifua kikuu, kutokwa na majipu, kutokwa uvimbe wa ajabuajabu katika mwili, kupatwa na mkanda wa jeshi, kupatwa na saratani na magonjwa mengine ya maambukizi. Huo ni mfano wa kundi moja la magonjwa ya maambukizi, lakini hata magonjwa mengine hatari kama shinikizo la damu, magonjwa ya moyo, magonjwa ya viungo, kisukari, macho, na mengine mengi, huwa ni matokeao ya ulaji wa vyakula visivyo sahihi au uachaji wa ulaji vyakula muhimu.
CHANZO CHA KUSHUKA KWA KINGA Ili uwe na kinga imara ya mwili, ni lazima uwe unakula mlo kamili unaojumuisha matunda, mboga za majani, nafaka na vyakula vingine vya asili, kwa sababu kila unachokula kina faida yake mwilini. Lakini siyo tu kula chochote kinachoitwa ‘chakula’, bali ule kilichosahihi na kilichosahihi. Katika maisha tunayoishi sasa, hasa mijini, idadi Kubwa ya watu hawali kabisa vyakula sahihi, badala yake wanakula vyakula ambavyo si tu ni hatari kwa afya zao, bali pia hudhoofisha kinga ya asili ya mwili na hivyo kuufanya mwili kubaki dhaifu na unaoweza kupatwa na ugonjwa wowote. Chanzo kikuu cha kushuka kwa kinga ya mwili kunasababishwa na ulaji wa vyakula visivyo sahihi ambavyo ndivyo vinavyopatikana kwa wingi kila mahali, hasa sehemu za mijini. Vyakula visivyofaa ndivyo vinavyotangazwa na kunadiwa kwenye vyombo vya habari kuwa bora. VYAKULA HATARI VINAVYOLIWA KILA SIKU Kuna orodha ndefu sana ya vyakula hatari ambayo huliwa kila siku, kuanzia asubuhi hadi jioni. Vyakula hivi yumkini huliwa kwa takriban maisha yote ya mtu na huonekana ni vya kawaida.Baadhi ya vyakula hivyo ni kama vile unga wa ugali, mkate, chips na juisi. UNGA WA UGALI Unga wa ugali unaotumiwa na watu wengi nchini ni sembe nyeupe. Chakula kikuu katika kaya nyingi zinazotumia ugali kama mlo wa kila siku huwa ugali mweupe uliotokana na mahindi yaliyokobolewa na kusafishwa, kisha kusagwa na kutoa unga safi mweupe. Kwa mtizamo wa macho na ladha ya mdomoni, wengi wanaamini kuwa ugali wa aina hii ndiyo mzuri na unaotakiwa kuliwa. Ulaji wa ugali wa aina hii hauna faida yoyote mwilini, kwani hauna virutubisho,kwa sababu vilishaondolewa vyote wakati wa kukoboa. Virutubisho muhimu vya muhindi viko kwenye kiini chake, hivyo unapokiondoa unakuwa umeondoa lishe muhimu. Ndiyo maana hata panya hawali mahindi yaliyokobolewa. Kwa faida ya afya zetu na kwa ajili ya kuimarisha kinga ya miili yetu, sote tunatakiwa kula ugali wa dona, mtama au ulezi kabla hata ya kuugua. Vyakula hivi ni muhimu sana na siyo vya kimasikini kama ambavyo watu wengi wanadhani. Kwa bahati mbaya, upatikanaji wa unga wa dona umekuwa mgumu na ghali kuliko sembe nyeupe, hivyo kuwafanya watu wengi kukimbilia sembe nyeupe ambayo inapatikana kirahisi kila kona ya nchi na kwa bei nafuu. Kwangu mimi naliona tatizo hili ni la kitaifa na kisera. Serikali kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, ilipaswa kutoa elimu ya kutosha ya kuelezea madhara yatokanayo na ulaji wa sembe nyeupe kisha kuweka sera itakayokataza uzalishaji wa kibiashara wa sembe nyeupe kama ilivyo sasa. Sera ya namna hii ingeokoa maisha na afya za Watanzania wengi wanaoteketea kila situ kutokana na ugonjwa wa kisukari. Naamini kaya nyingi nchini hazijui kabisa kama ugali utokanao na sembe nyeupe wanaokula kila siku iendayo kwa Mungu, una madhara kiafya. Ni vigumu kuzieleza na zikakuelewa familia ambazo kwa maisha yao yote zimekuwa zikiamini kwamba kula ugali mweupe ndiyo kitu bora. Serikali ilipaswa kuliangalia suala hili na kuona kama janga la kitaifa, ilipaswa kuanzisha kampeni maalum ya kutoa elimu kuhusu vyakula na lishe kwa njia mbalimbali, zikiwemo za matangazo redioni na kwenye televisheni.
ULAJI WA MATUNDA NA MBOGA Hakuna kitu muhimu kwa mwili wa binadamu kama kujenga kinga ya mwili. Mwili unapokuwa na kinga imara, si rahisi kuugua magonjwa ya ajaba. Miongoni mwa kazi nyingi za matunda na mboga za majani, ni pamoja na hiyo kazi ya kujenga mwili na kuujengea uwezo wa kujikinga wenyewe. Pamoja na umuhimu huo, ni watu wachache sana hula matunda na kuyachukulia kama sehemu ya milo yao ya kila siku. Watu wengi hula matunda au mboga za majani ‘kwa bahati mbaya’, huona siyo chakula muhimu sana. Hili ni kosa kubwa miongoni mwa makosa mengi yanayofanywa na watu katika masuala ya afya. Matunda yanatakiwa kuliwa kila siku na kwa wingi, vivyohivyo mboga za majani. Unapoacha kula matunda na mboga za majani za aina mbalimbali, jua unaukosesha mwili wako kinga dhidi ya maradhi yanayoweza kujitokeza mwilini. VYAKULA HIVI NDIYO VINAVYOTUMALIZA
Vyakula tunavyotakiwa kuvila, hatuvili tena na pengine upatikanaji wake ni wa shida, hivyo tunalazimika kula vilivyopo licha ya kuwa vina madhara kwa afya zetu. Hali hii imeongeza idadi ya wagonjwa na magonjwa sugu. Chakula kikuu cha mijini ni chips, kuku, mayai, soda, juisi za makopo au paketi, nyama choma na pombe. Pia kuna mkate mweupe, maandazi na chapati. Vyakula hivi huliwa kila siku, lakini ukivichambua utagundua havina faida yoyote mwilini zaidi ya kuingia na kutengeneza maradhi.
CHIPS Chips ambayo kwa kawaida hutengenezwa kutokana na viazi mviringo na kukaangwa kwenye mafuta, ni chakula kinachotakiwa kuliwa kwa kiasi kidogo na kwa nadra sana, kwa sababu kiko kwenye kundi la vyakula vyenye mafuta mengi ambavyo huliwa kwa uchache sana.Lakini hali halisi ni kinyume chake. KUKU Kwa kawaida, kuku wengi wanaotumika kwenye biashara ni kuku wa kizungu. Nyama ya kuku hawa haina virutubisho sawa na kuku wa kienyeji. Hii inatokana na ukweli kwamba kuku wa kizungu hulishwa madawa mbalimbali ya kuwakinga na magonjwa na hulishwa vyakula vilivyochanganywa madawa ili wakue upesi. Kwa mazingira hayo, nyama itokanayo na kuku wa aina hii haiwezi kuwa bora. Kiasili kuku huishi mazingira huru kwa kula vyakula ambavyo hujenga na kuukinga mwili wake dhidi ya magonjwa mbalimbali, kuku wa aina hii ndiye anayefaa kuliwa na kuleta faida ya nyama ya kuku inayokusudiwa. MAYAI Halikadhalika, mayai yanayopatikana kwa wingi mijini ni yale yatokanayo na kuku wa kufuga. Kiasili, mayai ya kuku wa kufuga, hayawezi kuwa sawa na mayai yatokanayo na kuku wa kienyeji. Huhitaji kuwa mwanasayansi kuona tofauti kati ya yai la kuku wa kienyeji na kuku wa kufuga, kwani mayai hayo yakipikwa huwa tofauti kwa ladha na hata rangi. Ni ukweli ulio wazi kuwa kuku wa kufugwa hulishwa vyakula vya kutengeneza ambavyo ndani yake huwekwa kemikali na madawa mbalimbali, wakati kuku wa kienyeji hula vyakula asili kwa kujitafutia wenyewe na mazingira wanayoishi ndiyo yanayowafanya wawe tofauti na bora. Hivyo ni dhahiri kwamba mayai tunayokula ya kuku wa kizungu yana madhara zaidi kuliko faida mwilini. SODA Moja ya vinywaji vinavyopendwa na kutumiwa na watu wengi ni pamoja na soda. Matangazo mengi ya biashara yanafanyika kutangaza kinywaji cha soda na kuonesha kuwa ni kinywaji ambacho hakina madhara kabisa kwa mtumiaji. Kwa matangazo hayo na kampeni hizo, familia nyingi zimeamini kuwa soda ni kinywaji bora na hata watoto wetu wamerithishwa imani hii. Lakini kwa upande wa pili wa kinywaji hiki, siyo kinywaji salama kama ambavyo imekuwa ikielezwa. Siwezi kusema moja kwa moja kuwa mtu huruhusiwi kabisa kunywa soda kama vile ni sumu, lakini watu walitakiwa kuelimishwa na kuelezwa madhara ya kupenda kunywa soda na athari anazoweza kuzipata mtu kiafya. Naamini tahadhari inayotolewa kwa wanywa pombe, hata kwa wanywa soda ilipaswa kutolewa pia. Utafiti unaonesha kuwa soda, pamoja na vikorombwezo vingine, huwekwa sukari nyingi kiasi kisichopungua vijiko sita katika chupa moja. Kiwango hicho cha sukari ni kingi zaidi ya mara tano ya kile kinachoruhusiwa kwa mtu kutumia kwa siku. Na madhara ya sukari mwilini ni mengi, yakiwemo ya kudhoofisha kinga ya mwili na viungo kwenye sehemu za maungio na pia huongeza uzito wa mwili. Ukitaka kujua soda ina madhara kiafya, fanya utafiti binafsi na utagundua haya ninayoyaandika. Kunywa soda zisizopungua tatu kwa muda mfupi, kisha lala usiku kama kawaida halafu wakati wa kuamka asubuhi, usikilize mwili wako.Utaamka ukiwa na maumivu mwili mzima, utajihisi uchovu, hasa sehemu za maungio, mfano wa mtu aliyefanya mazoezi mazito au kazi nzito siku iliyopita. Hiyo ni kutokana na kuingiza kiwango kingi cha sukari mwilini.
JUISI Katika hali ya kawaida, juisi ni kinywaji baridi kisicho na kilevi wala madhara kwa mnywaji. Lakini utakuwa sahihi ukizungumzia juisi zilizotengenezwa kwa matunda halisi bila kuongezewa vitu vingine. Katika zama hizi, hali iko tofauti, juisi nyingi tunazodhani ni vinywaji baridi visivyo na madhara kwa afya zetu na za watoto wetu, hali haiko hivyo. Juisi nyingi zinazouzwa kila sehemu ni feki. Ni jambo lakusikitisha kuona jinsi binadamu anavyojaribu kushindana na Mungu kwa kutengeneza vitu vinavyofanana na vile alivyoumba Mwenyezi Mungu kwa ajili yetu. Juisi nyingi hutengenezwa kwa kuchanganya maji, sukari na rangi zilizotengenezwa kwa kemikali mbalimbali zikiwemo zenye ladha ya matunda. Juisi za aina hii ndiyo nyingi na zinapatikana kila kona ya nchi hii, waathirika zaidi wakiwa watoto wetu ambao hupenda kunywa kwa kufuata utamu wa sukari nyingi zilizowekwa na ladha za matunda. Utafiti umeonesha kemikali (Additives) zinazowekwa kwenye vinywaji hivi, hudhoofisha kinga ya mwili na huwa chanzo cha magonjwa ya saratani na mengine hatarishi. Nakusihi kuacha kunywa kabisa juisi hizo na usimpe mwanao, unamuua. Ukiacha hizo juisi zinazotengenezwa kwa kutumia kemikali ‘mwanzo mwisho’, kuna juisi zingine zinazodaiwa kutengezwa kutokana na matunda, zipo za ‘machungwa’, nanasi’, ‘pasheni’, n.k. Yapo makampuni pia yanayojitapa kutengeneza juisi zao asilimia 100 kutokana na matunda na kwamba hakuna kinachoongezwa kingine. (100% fruit, No sugar added au No additives, huandika hivyo kwenye maboksi yao au makopo wanayoweka juisi. Hata hivyo, utafiti wa hivi karibuni umeonesha kuwa makampuni mengi yanadanganya walaji. Kwa sababu siyo kweli kwamba hawaongezi kitu kingine katika utengenezaji wa juisi zao za matunda. Imejulikana kuwa huweka vitu vya kufanya juisi ya kwenye boksi au chupa ikae kwa muda mrefu bila kuharibika, halikadhalika huweka vitu vya kuifanya juisi hiyo kuwa na ladha moja. Acha nikupe mfano. Katika hali ya kawaida, ukichuma machungwa matano ya mti mmoja, lazima yatakuwa na ladha tofauti, yote hayawezi kuwa na ladha sawa japo yote yanatoka mti mmoja. Kwa maana hiyo, kama ukitengeneza juisi kwa kutumia machungwa yaliyochumwa kutoka miti tofauti, ladha ya juisi lazima itatofautina. Lakini utashangaa kuona ladha ya jusi za maboksi zote zinafanana. Wanachofanya ni kuweka ladha moja kwenye utengenezaji wa juisi zao kabla ya kupeleka kwa mlaji. Halikadhalika, juisi ukishaitengeneza, haiwezi kukaa kwa muda mrefu bila kuharibika. Kwa hiyo, ili kuifanya juisi hiyo iweze kukaa kwa muda mrefu bila kuharibika, lazima iwekewe kemikali ya kuihifadhi isiharibike.Kwa kuongezewa vitu hivyo, hata kama Kwa maelezo hayo, hatushauriwi sana kunywa juisi hizo ‘ready made’ kwa sababu zimekosa uhalisia, kwani zina madhara kwa afya zetu, licha ya maelezo na matangazo mazuri tunayopewa na watengenezaji. Badala yake tutengeneza juisi majumbani mwetu wenyewe kwa kutumia matunda halisi ili kupata faida katika miili yetu. Jiepushe na matumizi ya sukari nyingi katika juisi unayoitengeneza mwenyewe, kwani kwa kufanya hivyo utakuwa unaiharibu, weka sukari kidogo sana ikiwezekana acha kabisa.

HEBU TAFAKARI HAYA KWA KINAaaaa.....

1. Maisha yako yanaweza kubadilishwa kwa muda mfupi na mtu hata usiemjua. 2. Watu wenye furaha pengine hawana kila kitu cha kuwapa furaha ila kile kidogo walichonacho hukipa maana ya kukifurahia.3. Wapenzi wawili wanapogombana haimaanishi hawapendani,vivyohivyo wasiogombana haimaanishi wanapendana. 4. Unaweza kufanya jambo fulani la muda mfupi lakini likakunyima furaha milele .5. Unapoagana na uwapendao waache na maneno mazuri pengine inaweza kuwa mara yako ya mwisho kuwaona. 6. Inaruhusiwa kuwa na hasira ila haimaanishi uwe katili.7. Ukomavu wa mtu huja kutokana na changamoto alizozipitia kwenye maisha na kujifunza kupitia changamoto hizo na sio umri aliouongeza. 8. Wakati mwingine inatosha kusamehewa na wengine,ifike mahali ujifunze kujisamehe mwenyewe. 9. Sio lazima uwe na kiherehere cha kujua siri flani pengine kuijua kunaweza kubadili maisha yako milele. 10. Watu wawili wanaweza kutazama kitu kimoja lakini kila mmoja akaona tofauti

Thursday 18 October 2012

Je wajua kicheko ni Tiba ya Ukweli?

Utafiti umeonyesha kwamba faida ya kucheka ni kubwa na inayofaa kwa afya ya mwili na akili. Watafiti hadi sasa wamedokeza kuwa kicheko husaidia kupunguza maumivu, kuleta furaha zaidi, na hata kuongeza kinga. Kicheko kwa hiyo, ni dawa isiyo na gharama ambayo kila mmoja anaweza kuipata. Kinachotakiwa ni kujenga mazoea ya kufurahi na kujitahidi kuwa na hisia ya ucheshi mara kwa mara. Faida za kicheko: 1.Homoni: Kicheko hupunguza kiwango cha homoni zinazoleta msongo(stress) kama cortisol na epinephrine dopamine (Adrenaline). Pia huongeza kiwango cha homoni ya kuimarisha afya kama endorphins na neurotransmitters. Kicheko husababisha kuongezeka kwa idadi ya seli za kinga (antibody); pia huzalisha na huongeza ufanisi wa seli T. Yote hii ina maana kuwa mfumo wa kinga mwilini huimarika, na hupunguza uwezekano wa msongo wa mawazo(Stress). 2.Mwili kujiachia(Physical release): Baada ya kicheko akili na mwili hupata hisia nzuri, ni kama unajiachia 3.Utendaji wa ndani Kicheko hutoa mazoezi ya kiwambo (diaphragm), husaidia mabega (works out the shoulders) na kufanya misuli kushirikiana zaidi;lakini pia husaidia moyo(provides a good workout for the heart). Kicheko pia huondoa hasira, hatia, dhiki na hisia hasi. 4.Kijamii Kicheko hutuunganisha na wengine. Kucheka hujenga mahusiano mema na huleta kuaminiana.Furaha na faida ya kicheko huongezeka maradufu ikiwa watu wengi wanacheka pamoja.Kicheko ni njia nzuri ya kufahamiana na kushirikiana. Unaweza je kucheka: Kicheko ni moja ya tiba mbadala ya bure, urahisi na yenye manufaa kwa njia nyingi. Unaweza kupata zaidi kicheko katika maisha yako kwa mikakati ya ifuatayo: 1.Angalia vipindi vya TV vya kuchekesha pamoja na filamu za ucheshi. 2.Cheka na marafiki kazini,shuleni na hata nyumbani. Fanya kicheko kuwa tabia yako. 3.Acha kulalamika kuhusu maisha,jaribu kucheka. Kama jambo fulani linakuchanganya ni vizuri kuangalia nyuma juu yake na kucheka. Usikubali kusongwa na mawazo,zungumza na wenzako lakini juu ya yote angalia,soma au kumbuka mambo yatakayokuchekesha ! Wachaaaa nichekeeee mieeeee Haaahaaaa ahaaaaaaa....Yeeaaaaaahhh

Tuesday 2 October 2012

Sigara huharibu DNA mwilini na kuongeza hatari ya kupata kensa!

Kemikali za sumu zilizoko katika tumbaku ya sigara huharibu DNA za mwili wa binadamu dakika chache tu baada ya mtu kuanza kuvuta sigara. Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa hivi karibuni, kemikali hizo zinazoitwa Polycylic Aromatic Hydrocarbons (PAHs) husababisha DNA ziharibike na kuongeza uwezekano wa mtu kupata kensa. Katika uchunguzi huo watalamu walichukua kemikali hizo katika miili ya wavuta sigara na kuzifanyia uchunguzi, ambapo waligundua kuwa, kemikali za PHA hubadilika haraka mwilini na kuwa sumu ambayo huharibu DNA baada ya kupita dakika 15 hadi 30 tangu kuingia tumbaku katika mwili wa binadamu. Sumu hiyo hubadilisha seli mwilini au kufanya mutation, kitendo ambacho huweza kusababisha kensa. Wataalamu hao wanasema, kitendo hicho hufanyika kwa haraka sana kama vile inavyoingizwa mada ya sumu kwenye damu kwa sindano. Habari hii ni tahadhari kwa watu wanaotaka kuanza kuvuta sigara, kwani takwimu zinatuonyesha kwamba, watu 3,000 hufariki dunia kila siku umwenguni kutokana na kensa ya mapafu, maradhi ambayo husababishwa kwa asilimia 90 na uvutaji sigara. Madhara ya kuvuta sigara kwa muda mrefu yanajulikana na wengi, ambayo ni pamoja na magonjwa ya moyo na kensa mbalimbali, lakini wataalamu wanatuasa ya kuwa, madhara ya sigara huanza pale tu mtu anapoanza kupiga pafu ya kwanza na kuingiza moshi wa sigara mwilini. Hivyo bado hujachelewa na unaweza kuacha sigara hii leo!

Tuesday 25 September 2012

Watanzania mabingwa wa kiswahili?

Kwa mpenzi yeyote wa Kiswahili ni sharti azingatie stadi nne za lugha hiyo. Yaani kuzungumza, kusoma kuandika na kuelewa lugha ya Kiswahili. Hata hivyo baadhi ya wakenya wamekuwa wakilamika kuwa vitabu vingi vya Watanazani vimekuwa vikitahiniwa nchini Kenya hususan katika vidato vya tatu na vinne. Ukweli ni kuwa Watanzania wamewabwaga wakenya na ipo mifano ya kutajika kuhusiana na hilo katika vitabu hususan vya fasihi. Swali ni je Wakenya wamepewa fursa ya kuandika au la? Ni nani anastahili kuwaambia waandike vitabu vya Kiswahili, na je wachapishaji vitabu wako radhi kuzichapisha kazi za Wakenya? Kuanzia miaka ya themanini hadi sasa, idadi ya vitabu vya Watanzania vilivyotahiniwa katika kunga za riwaya, tamthilia na ushairi ni kubwa kushinda vya Wakenya. Riwaya ya Kusadikika ya Shaaban Robbert(Mtanzania) ilitahiniwa mwanzoni mwa miaka ya tisini hadi mwaka 1994. Wakati huo hadi mwaka 1997 tamthilia ya Mashetani ya Ebarahim N. Hussein(Mtanzania) ilitahiniwa. Mwaka wa 1994 hadi mwaka 1998 riwaya ya Kisima cha Giningi ya Mohamed Said Abdullah(Mtanzania) ilitahiniwa. Katika miaka hiyo kuanzia mwaka 1998 tamthilia ya Amezidi ya Said Ahmed Mohamed (Mpemba) ikaanza kutahiniwa kuchukua mahali ya tamthilia ya Buriani ya A. S Yahya na David Mulwa(Wakenya). Wakati huo Mkenya Khaemba Ongeti alijipenyeza na tamthilia yake ya Visiki. Hayakuishia hapo, baada ya tamthilia za Visiki na Amezidi kuondolewa katika ratiba ya shule za upili nchii Kenya ikaingia riwaya nyigine ya Mohamed Said Ahmed (Mpemba) ya Kitumbua kimeingia mchanga. Na hiyo ilipoondoka ikaja riwaya ya Utengano ambayo inatahiniwa hadi sasa. Ukweli unaojitokeza hapa ni kuwa taasisi ya elimu nchini haiviteui vitabu hivyo kwa sababu ni vya Watanzania. Ni kutokana namna vilivyosukwa kimaudhui na kifani.Isitoshe waandishi wa vitabu hivyo wameandika wameandika vitabu vingi tu. Kwa mfano Said Ahmed Mohemed ameandika zaidi ya vitabu 40 vya Kiswahili. Mohamed Said Abdullah ameandika vitabu vingi tu kama vile Kisima cha Giningi, Duniani kuna watu, Mizimu ya watu wa kale na Kadhalika. Hata hivyo ni vyema kutambua kuwa baadhi ya Wakenya wamejitokeza na kuandika kazi nzuri za fasihi ya Kiswahili kama vile Siku Njema ya Ken Walibora, Mstahiki Meya ya Timothy Arege na Kifo Kisimani ya Kithaka Wamberia. Kwa ufupi wapenzi wa Kiswahili katika kanda ya Afrika Mashariki wakijumuisha mataifa ya Rwanda, Sudan Kusini, Sudan, Somalia na Uganda waandike vitabu zaidi vya Kiswahili. Twasubiri siku watanzania watavitahini vitabu vya Kiswahili vya wakenya, Vivyo hivyo si dhambi kitabu cha Kiswahili kilichoandikwa na Mrundi ama Mnyarwanda kikitahiniwa Uganda na vinginevyo. Ni maoni tu!!!!

USOMAJI WA VITABU WAPUNGUA KWA SABABU YA MITANDAO YA KIJAMII???

Nimejikuta natafakari jambo hili na kuingia kwenye marumbano makubwa na serikali ya kichwa changu hasa nikiangalia hali halisi tunayoishi sasa. Mapinduzi ya kompyuta yamebadilisha sana maisha. Enzi zile hata ukipewa assignment darasani unakimbia maktaba kutafuta kitabu. Siku hizi mambo yamebadilika. Hata assignment inapotolewa wanafunzi wanakimbilia kwenye Internet maana vitu vinapatikana kwa urahisi zaidi. Najiuliza kwa staili hii kweli watu hasa walio na access ya Internet wastani wao wa kusoma vitabu ukoje? Ripoti moja ilishawahi kuonyesha kuwa ujio wa smartphone na mitandao ya kijamii inawashawishi sana watoto wasome vitabu. Ilinipa wakati mgumu sana kuitafakari ripoti hii iliyotolewa kutokana na utafiti mmoja nchini Marekani. Nikiangalia mazingira yetu inanipa wakati mgumu sana kuamini jambo hilo. Naona kama vile uwezo na hamu ya watu kusoma vitabu unapungua zaidi wakipendelea kuingia mitandao ya kijamii kwa ajili ya kusoma hiki na kile! Hii ndiyo Teknolojia Yetu…

Sunday 23 September 2012

HUTOKA KIWALENIIii HIKI HAPA KICHWA KINGINE...(KIWA WA 2)ANAWAKILISHA DH CREW-MWITE HUBE KIWA...

SIKILIZA NGOMA YAO HAPAA INAITWA SIKUDHANI...
HUBE KIWA(sapremo wa kili)ANAWAKILISHA DH.CREW(ODEO & HUBE)

Tuesday 18 September 2012

TAHADHARI KWA WATUMIAJI SIMU ZA MKONONI

Simu zinatumia Mionzi ya MICROWAVE ambayo huwezesha kuunganisha simu yako kwenda kwenye Mnara na mnara huunganisha Simu yako na Mitambo ya Mtandao wako ambapo pia Hurudishwa kwenye mnara hadi kwa mtu Unaye mpigia. Microwave ndio njia kuu ya muunganisho huo Lakini kunamdhara mengi mtu huyapata kutokana na kuwa karibu na Mionzi hiyo ambayo hadi sasa bado haijafahamika ni kwa kiasi Gani. Uchunguzi umeonyesha kuwa kuna madhara mengi ya kiafya tunayapata kutokana na Matumizi ya simu. mfano wa magonjwa hayo ni 1.KUUMWA KICHWA MARA KWA MARA 2PRESSURE YA KUPANDA NA KUSHUKA 3.UVIMBE KWENYE UBONGO 4.KANSA 5.ALZHEIMER 6.NA MENGINE MENGI Hatuwezi kujizuia kutumia simu na Hatuwezi kuzuia hiyo mionzi ya MICROWAVE sababu ni sehemu ya shughuri zetu za kila siku ila tunaweza KUPUNGUZA. hapa nawaletea Njia chache za kupunguza Mionzi ya MICROWAVE isituletee matatizo makubwa zaidi. 1.Punguza matumizi yasio lazima ya simu. Mfano Ongea mda mfupi kwa kutumia simu sio muda mrefu uweunaongea,Uchunguzi umeonyesha kuwa ukiongea kwa DAKIKA mbili haileti madhara, (Alter natural electricity of the Brain) 2.Watoto wasiruhusiwe kutumia Simu bali pale tu inapobidi. 3.Tumia Earphone za wireless mfano za bluetooth. ni nzuri zaid kuliko za wire,Earphones za wire zinaongeza wingi wa mionzi sababu pia zinatumika kama antena ya simu, 4.Usiweke simu kwenye Mfuko wa suruari au shati au kiunoni,sehemu za mwili zinapitisha mionzi vizuri zaidi sababu pia ni njia ya neva za ubongo na chini ya mwili. 5.Usitumie simu kwenye chumba kidogo au lift au gari. Sababu Simu itatumia nguvu nyingi kuvuta mionzi ili kuwezesha mawasiliano. 6.Ukipiga simu subiri hadi mtu apokee ndipo uweke sikioni kusikiliza na sio wakati ina connect. 7.Usipige simu kama network ipo chini au signal inaonyesha bar moja au ndogo, simu itavuta mionzi zaidi ili kufanya mawasiliano 8.Ukinunua simu hakikisha unasoma kama ina LOW SAR (Specific Absorbtion Rate) Ni kipimo cha kupokea mionzi ya simu Za nokia zinazo ila za Kichina HAZINA. 9.Tumia vifaa vya kupunguza Mionzi vinapatikana madukani (vinawakawaka taa hivi) 10.Weka simu atleast 3.4 inches kutoka kwenye sikio 11.Jitahidi kutumia Earphones muda wote unapotumia simu 12.Tumia speaker phone."Loudspeaker " 13.Text zaidi kuliko kupiga simu . 14.Jitahidi usitumie muda mwingi kwenye simu kama umeiweka kwenye sikio 15.Jitahid kuiweka mbali na reproduction organs zako hasa kwa wanaume ambao hatujapata watoto.

SIMU ZA MKONONI NA KANSA YA UBONGO: BALAA JINGINE KWA AFRIKA?

Kwa muda mrefu kumekuwa na mjadala mkali kuhusu nguvu za mionzi ya mnunurisho inayotolewa na simu za mkononi kama zinaweza kusababisha kansa ya ubongo ama la. Hatimaye Shirika la Afya Duniani limetoa tamko kuhusu utafiti unaoonyesha kwamba simu za mkononi zinaweza kuwa zinasababisha kansa ya ubongo. Hatari hii inasemekana kuwa ni kubwa zaidi kwa watoto wadogo na matineja kwani mafuvu yao bado hayajakomaa sawasawa. Naomba hii isiwe kweli kwani kama tunavyojua, Afrika ndiyo jalala la bidhaa feki, mbovu na zilizoisha muda wake. Bila shaka nitakuwa sahihi nikisema kwamba simu zinazotoa mionzi hatarishi kwa binadamu na zitakazokuwa zimepigwa marufuku sehemu zingine za dunia ndizo zitarundikana Afrika. Kama utafiti huu ni wa kweli basi miongo kadhaa tu ijayo Afrika itakumbwa na mripuko wa kansa ya ubongo – mojawapo ya kansa hatari kabisa na inayohitaji tiba ghali sana! Tunachoweza kufanya kwa sasa ni kufuata mapendekezo yaliyotolewa yakiwemo kununua simu zisizotoa mionzi mikali zaidi, kuweka simu mbali na sikio wakati wa maongezi na kwa wenye uwezo kununua vifaa vinavyosafirisha mawimbi ya sauti kama “Bluetooth”. Vifaa hivi huwekwa sikioni na vinaweza kudaka mawimbi ya sauti ya simu iliyowekwa mfukoni au sehemu nyingine na kuyasafirisha sikioni kwa msikilizaji bila madhara yo yote.

Monday 17 September 2012

Elinaja kijana aliyeamua kuandika bongo fleva kwenye mtihania atoa single yake mpya akimshirikisha barnaba.


Bado Tanzania haijamsahau huyu mwanafunzi ambae aliongelewa sana wakati matokeo ya form IV yalipotoka mwaka jana kutokana na kuandika mistari ya bongofleva kwenye mtihani wake baada ya kuona hakuna chochote alichopata kwenye elimu.
Elinaja alisema  aliamua kuandika mistari ya bongofleva ili wahusika wapate msg, hata hivyo alisema kitu ambacho ana uhakika uwezo wa kukifanya anao ni muziki ambapo amerekodi upya single yake ya Mr President na kumshirikisha Barnaba, bonyeza play hapo chini kumsikiliza na kudownload.

Monday 10 September 2012

Faida za Tende Mwilini Mwako.

Je unajua kwamba tende ndio tunda pekee lenye kuupatia mwili vitu vinne kwa wakati mmoja, vitamin,protini,wanga na mafuta?. Mbali na utamu wake tende ambazo hulika sana Mwezi wa Ramadhan zina faida nyingi sana kwa mwili wa binadamu. Ebu zijue faida zake……. Tende ni tunda ambalo linayeyuka kirahisi tumboni, na lenye faida nyingi sana ambazo hulifanya liwe tunda la kipekee. Baadhi ya faida zake mwilini ni kama ifuatavyo: 1-Kwa watu wenye matatizo ya tumbo, nicotinic inayopatikana kwenye tende,husaidia kurekebisha matatizo ya tumbo na huleta ahueni kwa watu wenye matatizo ya kupata choo. 2-Tende husaidia kuuimarisha moyo. Iloweke tende kwenye maji kwa usiku mmoja na asubuhi kunywa maji hayo pamoja na tende zilizolewekwa baada ya kuondoa mbegu,ukifanya hivyo mara mbili kwa wiki,moyo wako utakuwa imara. 3-Tende husaidia pia kwenye mambo ya malavi davi. Iloweke tende kwenye maziwa ya mbuzi usiku, asubuhi changanya maziwa hayo na asali,kisha kunywa, njia hii husaidia kuongeza nguvu na stamina za kufanya mapenzi. 4-Utafiti umeonyesha kuwa tende husaidia kutanua misuli ya mji wa mimba,wakati mwanamke anapokaribia kujifungua,hii husaidia kumfanya mwanamke asipoteze damu nyingi wakati wa kujifungua. 5-Wataalamu wa vyakula, wanazichukulia tende kama chakula bora kwa wanawake wanaonyonyesha,kwani husaidia kuyapa maziwa virutubisho muhimu vinavyomfanya mtoto awe na afya njema. 6-Tende husaidia kupunguza kiwango cha kilevi (alcohol) kwenye damu. Maji ya kunywa ambayo tende imelowekwa ndani yake husaidia kuondoa haraka alcohol mwilini. 7-Tende husaidia kuchelewesha dalili za uzee,na pia husaidia kurekebisha ngozi na huondoa mabaka ya kuungua na jua. 8-Kutokana na madini ya chuma kwenye tende,watu wenye upungufu wa damu hupata ahueni. 9-Vitamin B1 na B2 zilizopo kwenye tende,husaidia kuyapa nguvu maini. 10-Tende pia huleta ahueni kwa watu wenye kikohozi na mafua.

Tuesday 21 August 2012

BARUA KWA VIVIAN TILLYA FROM teamSUA-HIP HOP



 Dear Vivi....


Ni miaka saba sasa tangu uondoke na tunakukumbuka sana michano yako na mambo mengine mengi....(jalini ubinadamu msifanye mavitu kama sanamu.....). Natumai umeonana na Faza Nelly,DOG Nacko.Papaa,Mlost na Pacha Izzy na wengine wengi waliokuja huko.

Dhumuni la barua hii ni kukusalimu na kukujulisha yanayoendelea Arusha.
Mengi yametokea ila ya Muhimu kukufahamisha kuhusu harakati za Muziki hapa Arusha.
Imagine eti siku hizi Metropole,Ricks,Mawingu na Crystal club hazipo tena.
Machizi wengi wamehamia Dar es salaam(just like you...) ila wao wamebadilisha hadi majina wanakuja Arusha kufanya show na kusepaz.
Machalii wapya kibao kwenye Game na wanakalisha usipime wengine wako mbele na wanafanya harakati zilezile Kzz wa X plastaz hajarudi bado tangu aende na anatoa Mixtape moja kali sana hivi karibuni,Chindo pia anawakilisha akiwa huko si unajua tena Jamaa alivyo mbishi.
Jcb na Spark bado ni hardcore(...wana makid asee).

maprodyuza wengi wapya na Studio nyingi.WATENGWA kuna Daz Naledge,DX amekuja na Noizmeka,hata Ngalimi siku izi kuna Studio asee KZ kaja na KAZAWAZA.Grandmaster siku izi wanapiga mpaka VIDEO bana.zipo mingi siwez hata kuzitaja zote.

Harakati zote zile za rap sasa hivi zimeamia Kijenge ya Juu(S.U.A Free-Stage

Watu kibao wanakutana na kupiga freestyle,michano na magrafiit kibao.

Si unakumbuka vile ulikua ukikasirika kuona hakuna mademu kwenye HIPHOP concert na ukawa unaamua kuonyesha uwezo wako dah! ulikua unakalisha asee(.....sa nani wakuongoza safari wote tunaujua usukani.......siwaelewi! )
Juzi si kuna madem wakaibuka SUA bana asee tulikukumbuka sana laiti ungekuwepo ungefarijika kinyama.

Kuna redio stesheni mingi niaje! karibu kila mtaa na maclub za kutosha huko town usiku kama tu mchana. ... kuna masista Dread wengi peace kama wewe.... inapendeza

Arif mambo kibao yamebadilika... kutoka TAPE na disc man siku izi kuna mavitu yanaitwa I-pod,I phone na ma-I pad kitu touch screen maamaaa si unajua Swagga tena...(sorry i know you now know about Apples kama sio matunda tena nikikuambia mambo ya Blackberry si ndo utadata kabisa...hahahahaha!!)

I will tell you about it next time sahivi naenda misele so kama vipi mpe hi Complex(Mwambie alivyosepa tu BTOWN CLAN wakaNYAMAZA ooh SH**T MIKOSI WAMENYAMAZA.....),James Dandu,Drob,Steve2k,produza Roy na wengine mlioko nao huko.

Jumapili tarehe 26 SUA itakua ni spesho kwako na Complex wa2 watapiga mistari yenu..oooyyyy! .Nitakujulisha zaidi next time.

Wako Wapendwa
Katika HIP HOP
###teamSUA###


VIVIAN TILYA  ALIFARIKI DUNIA 21AUGUST KWA AJALI YA GARI ILIYOTOKEA MBWEWE AKIWA NA COMPLEX.

UNAKUMBUKWA NA FAMILIA YAKO NDUGU JAMAA NA MARAFIKI.

NAAMINI UMEKUTANA  NA FREDY JEBI, FATHER NELLY, MLOST NA PACHA ONE.

TUTAZIDI KUWAKUMBUKA..BWANA ALITOA NA BWANA ALITWA UPUMZIKE KWA AMANI VIVIAN.
AMENI.........



Saturday 11 August 2012

Exclusive: Makala ya kusisimua kuhusiana na maisha magumu ya mdogo wake Obama



Obama's slumdog brother: Kutana na mlevi asiye na matumaini aishie jijini Nairobi ambaye ni mdogo wake na rais wa Marekani


Makala hii imetafsiriwa kutoka kwenye gazeti la Daily Mail mwandishi akiwa  ANDREW MALONE. Makala hii imechapishwa jana, August 10, 2012.

Wakati mwanaume mrefu na anayejulikana sana akiondoka kwenye kibanda chake kilichopo kwenye makazi fukara kabisa barani Afrika wiki hii, baadhi ya watu walianza kumuita kwa utani:‘Mister President! Mister President!’

Akielekea kupata kifungua kinywa huku akivuka mifereji inayotiririsha maji machafu, muonekano wa jamaa huyu mrefu na aliyekonda, unavutia vicheko vya chini chini kutoka kwa watoto wanaocheza kwenye jalala.

              George akiwa kwenye nyumba anayoishi

Jina la jamaa huyu ni George Hussein Obama, ni mdogo wake na Barack Hussein Obama, rais wa kwanza mweusi wa Marekani na mwanaume anayeheshimika zaidi duniani.





Wanaume hawa wawili wanachangia baba lakini Barack Obama alizaliwa Hawaii kwa mke wa pili wa baba yao ambaye ni mmarekani na George alizaliwa nchini Kenya akiwa mtoto wa mke wanne wa mzee huyo.

Leo, wakati Barack akifurahia maisha kwenye Ikulu ya White House, akiruka kwenda nje na Air Force One na ni rafiki wa mastaa wa filamu na wengine mashuhuri, George, 30, anapatikana akiwa amechoka kwenye makazi yake ambayo hata wakazi wenzake wa eneo hilo maskini jijini Nairobi wanayaona kama kichuguu.




Ingawa anadai kutotumia heroin au cocaine, George hutumia muda mwingi kunywa Gongo (Chang’aa) kuanzia anapoamka mpaka muda ambao huanguka na kuzima kabisa.

Gongo anayokunywa ni ile iliyochanganywa na kemikali ya ethanol, na kuongezea acid kutoka kwenye betri ili kuipa kick zaidi, na mchanganyiko huu husababisha upofu na kifo inapochanganywa vibaya.

Kiasi kidogo tu cha pombe hiyo huwafanya hata wanywaji wazoefu kulewa kiasi cha kushindwa hata kukumbuka majina yao. Wanywaji wa mara kwa mara huathrika maini na figo ama ubongo.


Nilipomtafuta George asubuhi siku moja kufahamu maisha yake, alikuwa tayari kwenye kibanda kimoja jirani akinywa Chang’aa ambapo ngono na machangudoa ni sehemu ya menu na hufanyika kwenye kitanda kilichowekwa nyuma.

Utambulisho unafanywa na ‘mpambe’ wa George  — mkazi wa eneo hilo mwenye macho mekundu na mnywaji mwenzie ambaye anamvuta George nje ya kibanda hicho na kumwabia aje kumuona mzungu nje (shouting at him to come and see the ‘muzungu’ (white man) outside.

Baadaye baada ya kusalimia, ninafanya kosa. Namkaribisha George kwaajili ya chakula cha mchana kwenye hoteli yangu. Kwa siku mbili zilizofuatia, aliivamia baa yangu ndogo, kuwaalika wapenzi wake kibao na washkaji zake kula na kunywa kwa gharama zangu na kujionesha kama staa aliyeharibikiwa.

Aliomba pia ‘kitu kidogo’ — Swahili for something small, which, of course, means something large and financial — na alichukia baada ya mimi kukataa kuwapa hela mademu zake.

George pia aliendelea kulaumu kuhusu jina la Obama kuwa kama mzigo na laana kwake, ilhali wakati mwingine bila aibu hulitumia jina hilo kupata hela nyingi iwezekanavyo ili kuzitumia kunywa na kuvuta bangi.

‘Watu wanavutiwa na mimi kwasababu ya kaka yangu,’ anashusha pumzi na kushusha  Johnnie Walker mbili kwa mpigo. ‘Nachukia’. Watu wanapenda niwe mtu mwingine.’

Mara ya kwanza George alikutana na kaka yake alipokuwa shule ya msingi. Barack alienda Nairobi miake michache tu baada ya baba yao kufariki kwa ajali ya gari. George anakumbuka alikuwa akicheza soka wakati kaka yake alipowasili kumsalimia.

Mara ya pili wanakutana ni kipindi Obama — alipokuwa Senator na alifanya ziara ya Afrika Mashariki mwaka 2006, na kutembelea Nairobi kuiona familia yake.


George anasema kwa sasa watu wanamshinikiza afuate nyayo za kaka yake kwenye siasa. ‘Nina watu wengi ambao huniambia nigombee ubunge. Lakini sivutiwi na siasa.’

Kisha anatulia, na kuongeza: ‘Lakini kama Barack angekuwa rais na mimi ningekuwa rais wa Kenya ingekuwa rahisi kuonana.’

Anasema umaskini wake ndio unawazuia ndugu hao kuwa na uhusiano wa karibu.


‘Ana majukumu. Hatakiwi kunilea mimi,’ anasema. Mimi ni mtu mzima, kila mtu hudhani kuwa huwa ananitumia fedha. Lakini mimi sio ombaomba.’ Lakini alipoulizwa iwapo aatachukua fedha akipewa na Obama alisema: ‘Seriously! Yes! Who wouldn’t?’

George alikulia jijini Nairobi akiwa na mama yake ambaye aliolewa tena na mfaransa aliyekuwa anafanya kazi kwenye shirika la misaada jambo ambalo anadai lilimfanya awe hivyo.

Alianza kunywa pombe na kuvuta bangi akiwa na miaka kumi, miaka mitano baadaye alifukuzwa kwenye shule ya boarding, ambako alicheza rugby na kujifunza lugha za kigeni kutokana na kutumia madawa ya kulevya.

Anakubali kuwa alikuja kuwa addicted na cocaine na heroin akiwa na miaka 17, na kuwa mwizi wa kutumia silaha ili kupata hela ya kunywea pombe.

Mwaka 2003 alifungwa jela kwa kosa la kuiba kwa kutumia silaha.

Alikaa kwa miezi tisa kabla ya kutoka kutokana na kukosekana ushahidi.

Swali ni je! George anastahili kuishi maisha haya wakati kaka yake ni rais wa Marekani?

Friday 10 August 2012

LINEX AOMBA RADHI WANAWAKE WOTE NA JAMII KWA UJUMLA





siku chache baada ya msanii Linex kutoa video ya wimbo wake (AIFOLA), ameandika katika ukurasa wake wa facebook, akiomba radhi kwa wanawake wote kutokana na kipande cha video yake ikimuanyesha akimpiga kofi mschana aliekuwa anaigiza nae katika video hiyo kutokana na kupata malalamiko mengi yanayodai kuichochoa jamii katika vitendo hivyo hasa kwa wanaume

"Naomba radhi kwa kila mwanamke Dunian kofi nililompiga vdeo gal wa kwenye aifola vdeo sikua nakusudia uchochezi wa mwanamke kupigwa na mwanaume wake natumai wanaume wenzangu mmenielewa lengo ilikua kutafuta uhalisia wa matukio kwenye vdeo yangu #team mwanamke hapigwi analiwazwa na kubembelezwa..." amesema linex




KUTOKA KWENYE MUZIKI HADI TV,DRAMA INAYOITWA FX



Dr.Dre ni kati ya wasanii wa Hip Hop waliopata heshima sana katika game na alitajwa katika marapper watano wenye mkwanja akiwemo P.Diddy, Jay Z, Birdman, 50 cent na yeye mwenyewe Dr Dre. Katika mauzo ya headphones zinazofahamika kama beats by dre zilimumrudisha Dre hadi juu na kuwa kati ya marapper wenye mkwanja, Na kwa sasa yuko tayari kuanza kuonekana kwenye Tv Drama mpaka sasa bado anaendelea kumalizia script ya Drama FX.

SINTA:HUYU NI NANI?ETI MUIMBAJI?HAPATIKANI HATA GOOGLE AU NDIO WALE KIINGILIO BUKU UZINDUZI TANDALE





leo hii katika pita pita zangu, nimekutana na story hii iliyoandikwa kupitia sintah.com, ikionekana kuwa ni majibu kwa Ney wa mitego, baada ya kuongea kwenye Take one kuhusu single yake ya NASEMA NAO na kumtaja mwanadashosti Sintah kuwa anafanya chochote kile ilimradi arudi kwenye game...... na haya ndio majibu yaliyofumuka.....
hivi wa wapi weweee,mbona husomeki weweee,tume google
hupatikani wewe,shukurani kwa mdogo wako alietuletea picha yako ya beach, sijui nani sijui nay utaweza??
jipange,namuonea huruma mama yako kuzaa kiumbe
kilichoharibikiwa, nina jaribu ku google naona neyo wa Us sasa nisaidie nitupie kwa mnyamani au kiembe mbuzi niambieeee ili nikupate my brodaaaaa you have just tickled a private part of a tiger,,, you wanted promo now you gotta maza vitumbua 
NEY WA KUJITEGA MWENYEWE MAANA
UNA CHASTE  MBU SIJUI UTAMTEGA NANI, KAMA UNA SHIDA NA MIMI DJ DJ DJ AND MY BRODAA CHOKA ANAJUA NINAPOEGESHA MILONJO YANGU  SASA KAMA UNATAKA KUIKATA KAMA ULIVYOWAMBIA WATU WAKO BBM(MAANA HU HUNA HADHI YA KUKAA KTK MY BBM LIST) MWAMBIE AKULETE MDOMO HUPONZA KICHWA NA UMEJIPONZA LOVES LEO NIMEWAFUNGULIA COMMENT MTU AKIGUSWA ATAJIJUA MAANA NIMECHOKA KUONEA WATU HURUMA KAMA NOMA NA IWE NOMA
NEY NIMESHAMPA RUHUSA MLINZI AKURUHUSU UINGIE SWALI ANAKUJUA??? JIPANGE ULIPOCHOKOZA SIPO KABISA UNSTOPPABLE NOTHING BUT CONFIDENCE
MSICHANA AMBAYE ANA TWO SIDES (COOPERATE FIGURE NA ACTRESS) OOH SORRY USIJE MCHANA NITAKUWA SERENA NINA APPOINTMENT NA WORLD BANK CREW CONCERNING MY LAUNCH  

SINA SHIDA NA  MTU ILA UKINIANZA HUWA NAMALIZA  SHIDA ZAKO 
cc to naxylady upo kwenye cue usitafute maarufu maana umaarufu hauji kwa njia za panya from Unstoppable
MA International Relations & Diplomacy

Saturday 28 April 2012

AJALI YA BASI LA COAST LINE



Hili ni basi la Coast line ambalo limepata ajali siku ya leo Juma mosi asubuhi katika kijiji cha Terrat kilichopo wilayani Sianjiro Mkoani Manyara.


Basi hilo lilikuwa likitokea Mkoani Arusha likieleke Mkoania Dodoma,na ndipo lilipopata na ajali hiyo katika eneo la kijiji hicho baaada ya STALING kukatika na kusababaisha kuugonga mti uliokuwa kando ya bara bara hiyo na kupelea tairi za mbele zote 2 kupasuka.


Basi hilo limeharibika vibaya sehemu ya mbele upande kulia ambao huwa anakuwa Dreva,amabaye amevunjika mguu mara mbili na abiria wengine kupata majeraha mbali mbali.



           Hawa ni baadhi ya abiria walionusurika katika Ajali hiyo



Na huu ndio mti wa Mgunga ambao Basi hili la COAST LIME limeugonga baada ya Kukatika STALING.

By Kiwa Strong..

Wednesday 25 April 2012

KWA NINI VIUMBE WENGI WANA MACHO MAWILI

Nilikuwa natafakari juu ya uumbaji na kushangazwa na kitu kimoja cha ajabu; viumbe vingi hata vinavyoishi mazingira tofauti na vya aina (specie) tofauti sana vimefanana kwa kuwa na macho.


Vinaweza vyote visiwe na miguu, mbawa, au pua lakini karibu vyote vina macho. Kuanzia majini, angani na nchi kavu viumbe vingi vinamacho! Wadudu wadogo na wanyama wakubwa wote wana macho; samaki na ndege hadi minyoo ina macho! 

Na katika maajabu ndani ya maajabu ni kuwa viumbe vingi vina macho mawili (sijajua kama yupo mwenye jicho moja) na vile vingine vina macho mengi (compound eyes). Angalia mifano hii:

Angalia Nyoka:




Angalia Samaki:




Angalia Ndege:


Angalia Vipepeo


 


Angalia Mchwa





Angalia Nyangumi


Angalia Kaa:



Angali Nyani:




Kwanini?
Jibu la kisayansi ambalo hutolewa mara nyingi ni "evolution"; lakini kwanini "eyes"? Utaona viumbe vinafanana vitu vingi tu lakini mara nyingi tofauti ni idadi.


kwa mfano viumbe vingi vina miguu minne (wanyama) lakini vipo vyenye miguu sita (wadudu) na vingine havina miguu kabisa (nyoka na samaki); lakini vyote vina macho! Kwanini macho ni mojawapo ya viungo ambavyo vinaonekana karibu katika viumbe vingi zaidi kuliko viungo vingine? Na kwanini mara karibu zote macho hayo yanakuwa mawili siyo matatu au manne (kuangalia pembeni, juu na chini)? 

Monday 23 April 2012

NJIA KUMI KUSAIDIA KUPUNGUZA UNENE..

Kati ya sababu kuu zinazopunguza uhai wetu ni afya, unene na kutojua kujiangalia vyema.

 
1-ULAJI
Ipo mifumo miwili ya kula. Chakula unachokula na namna unavyokila.
Unavyokula.

Kuna kula vyakula vidogo vidogo vyenye madini, vitamini, mafuta nk mara nyingi kwa siku; au kula milo michache (mmoja au miwili) mikubwa ili kujaza tumbo. Ulaji mdogo mdogo husaidia afya na kuingia mwilini vyema kuliko ulaji mkubwa wa mara chache.

Tumbo lina musuli zinazofanya kazi kama mashine au mnyama. Gari likijaa sana hupata taabu kwenda. Punda hivyo hivyo. Ulaji mdogo mdogo unaosambazwa mara kadhaa kwa siku  ni bora maana mwili unachambua kila kitu kwa wepesi na haraka. Unapokula milo michache mikubwa unapalilia zaidi mafuta mwili.

(PENDEKEZO la kwanza.  Asubuhi, kunywa maji kwanza, matunda, kisha ndiyo chai na vitu vingine kama mkate au maandazi…)

Wapo wanaodai kwamba wanakula matunda na mboga...

Tatizo ni kwamba mipangilio  yao huwa ya makosa. Mathalan wengi hula matunda baada ya chakula. Vimeng’enya  chakula (enzymes) tumboni hufanya kazi namna tofauti. Mathalan vile vinavyonyambua matunda ni tofauti na vinavyomeng’enya vitu vigumu zaidi kama nyama au wanga.

Matunda hunyambuliwa haraka zaidi kuliko vyakula vingine. Hivyo ni bora kula matunda dakika10-20 kabla ya chakula. Ukila baadaye matunda hugeuzwa aina fulani ya pombe (fermented food) inayoelea tu juu ya chakula na kubakia kitu kingine badala ya kuingizwa haraka ndani ya damu kupitia utumbo mdogo, uwengu, moyo, ini, nk.

Tatizo jingine ni kupika sana mboga hadi zikapoteza nguvu.

Mseto wa vyakula pia ni muhimu. Kwa mfano vyakula vyenye uchachu (acid) na vile vinavyomumunyuka haraka (alkine) havitakiwi viliwe pamoja. Mfano ni matunda.

Matunda chachu kama machungwa, mananasi na maembe yatakiwa yawe pamoja; na yale laini zaidi:  ndizi mbivu, matikiti maji, mapapai, matufaha, nk yaende kivyake, maana yana mfumo tofauti, wa kumeng’enywa.

 

Chakula unachokula.....

Waafrika  hatuna tabia ya kula mboga mboga mbichi. Tunafuata ladha na mazoea kuliko thamani.
Bara letu lina mboga na vyakula bora kuliko bara lolote duniani lakini sisi tunakufa mapema na kwa utapia mlo kuliko wale wanaotoka nchi kame.

Ulaya nzima imejazana mboga mboga zinazoagizwa toka Afrika. Kenya na Tanzania zinauza mboga za maharagwe mabichi (green beans), matunda toka Afrika Kusini na Ivory Coast; nk. Waafrika tunapenda kujaza matumbo. Unene umekithiri hata wale walio matajiri waliosoma bado wanakufa kwa kisukari shauri ya kutokula mboga mbichi.

Ulaji wa mboga mbichi ni upi?

Ni mathalani ulaji wa salad. Tanzania tunaita kachumbari. Lakini si lazima iwe kachumbari ya nyanya, vitunguu na chumvi tu. Waweza kuchanganya matango, nyanya kwa maparachichi; au vitunguu saumu, giligilani na karote.

Huu mseto wa mboga mbichi ni mzuri ukienda na chakula chenye nyama za minofu na wanga (ugali, wali, ndizi za kupika nk). Ulaji wa wanga asubuhi, mchana na jioni kila siku huchangia sana katika unene.

2-UNYWAJI  MAJI
Waafrika hatunywi maji, hasa wanawake. Wanaokunywa maji zaidi ni wacheza michezo. Wengi wetu hunywa zaidi soda (vinywaji baridi kama Cocacola, Pepsi, Mirinda ,Tangawizi  na gesi za kisasa kama Red Bull) zilizojaa gesi inayoleta vidonda tumboni; na chai.

Kuliko maji. Na maji haya hutakiwa  dakika 10-20 kabla ya chakula au nusu saa kuendelea baada ya chakula. Ukila  chakula huku unasakatia maji huimanisha mtu una kiu.

Ulaji chakula na unywaji maji ni vitu viwili tofauti. Ila utawaona watu wanakula huku wakibugia maji. Unapokula chakula huku unabugia maji unapunguza nguvu za chakula, unajaza tumbo maji na kuchelewesha mmeng’enyo wa chakula (digestion).

Chakula kisipomeng’enywa vizuri kinaketi tu tumboni. Matokeo wengi wetu tuna  matumbo makubwa. Kama hufanyi mazoezi lile tumbo linakwenda pembeni (chini ya mbavu) hasa kwa watu wa makamo linaleta maradhi kama kisukari, kiungulia, kuvimbiwa, uyabisi wa tumbo, nk.


3-SUALA LA UMENG’ENYAJI

Chakula huanza kumeng’enywa au kusagwa (kwa lugha iliyozoeleka) mdomoni. Mate yako mdomoni ni chanzo cha uchambuaji chakula. Unapobugia chakula bila kutafuna sawasawa unasababisha mambo mawili.

Moja chakula kutochambuliwa vizuri, pili chakula kwenda kukaa tu tumboni, au kama kikipita hakisaidii lolote mwilini.

Utafunaji wa taratibu husaidia umeng’enyaji. Chakula kinapofika tumboni hukaa pale dakika ishirini. Hapo huchanganywa na asidi (ya manjano iitwayo Hydrochloric) inayokibadilisha tayari kupelekwa utumbo mkubwa, kupitia kongosho.

Kule uchafu utapelekwa chini na rutuba kusafirishwa na utumbo mdogo kuelekea katika uwengu, moyo. Moyo utadunda chakula kilichoshageuzwa damu kuelekea mwilini kufanya kazi na akiba hubakishwa katika ini.

Sasa kama usipotafuna vizuri, ukila huku unakunywa sana maji au vinywaji vingine chakula hakimeng’enywi vizuri. Ndiyo maana unawaona watu wengine wanakula sana lakini hawana afya.

Wanaugua ovyo ovyo, wanatoka jasho ovyo, wanajamba ovyo, wana matumbo makubwa, wanavimbiwa, wanakaa siku nyingi bila kwenda choo (inatakiwa mtu kwenda haja kubwa mara moja au mbili kwa siku) nk.

Misitu na hewa safi ya mimea

4-ULAJI WA VYAKULA VYA MAFUTA

Mafuta ni suala muhimu sana mwilini. Ila ulaji wake shurti uwe wa mpangilio. Yaani unaowiana. Lazima mtu uwe na wastani mzuri wa vyakula vya nguvu, yaani “wanga” (ugali, ndizi, wali, viazi mbalimbali, mikate, mahindi, nk), ujenzi yaani “protini” (mboga na nyama), “madini” (mbegu mbegu mbichi si za kukaanga sana na chumvi) na “vitamini” (matunda, maziwa, mayai, nk).

Waafrika tunapenda nyama. Nyama ni muhimu sana maana ina madini aina ya chuma (nyama nyekundu) protini,nguvu na mafuta. Ila mafuta yaliyoko katika nyama mara nyingi si mazuri shauri hayatoki, huganda.

Chukua nyama ya kuku na samaki ambayo huwa na ngozi. Wengi wetu hupenda sana kula ile ngozi ya wanyama hawa kwa kuwa tamu. Lakini haya ni mafuta mabaya.

Mafuta ya samaki lakini ni mazuri. Samaki anayo mafuta ya Omega-3 ambayo husaidia mwili na kinga maradhi mwilini.

Tunapokula nyama choma au ya kukaanga, lazima tule pia mboga za majani (mbichi) na si vizuri kula nyama kila siku. Kama huwezi kukaa bila nyama kila siku, fanya mazoezi ya mwili.

PENDEKEZO LA 3- Kula mbegu mbegu za korosho, karanga au mlozi (ziwe mbichi badala ya kukaanga na chumvi) kati kati ya siku. Haya ni mafuta yenye rutuba mwilini kuliko nyama za mafuta.


Chips za Magimbi

MAZOEZI YA MWILI NA VIUNGO

Mazoezi ni mfalme wa kupunguza unene.

Ukiwauliza wengi watakuambia wanafanya kazi ngumu za sulubu (wanachuruzikwa jasho) kwa hiyo hayo ni mazoezi. Ila kazi na mazoezi ni vitu viwili tofauti. Ingekuwa kufanya kazi ni mazoezi basi kusingekuwa na wastani mfupi wa maisha kwa maskini hasa sisi Waafrika.

Wengine watadai kwamba walipokuwa wadogo shuleni walifanya mazoezi sasa wamekuwa watu wazima (miaka 40 kuendelea) kwamba eti mazoezi ni suala la ujana; kumbe kadri unavyokuwa ki umri ndivyo kadri unavyotakiwa kufanya mazoezi na kujitazama zaidi kiafya.

Watazame Wachina na Wajapani wanavyoishi maisha marefu.

Mazoezi ni shughuli inayokufanya kwanza uheme (mapafu na moyo kwenda kasi), viungo na mifupa kujinyoosha (stretching), kutoka jasho na usafishaji wa damu.

Mazoezi yanayosaidia haya ni pamoja na kutembea kasi, kukimbia, kuogelea, michezo mbalimbali ya riadha (kama mpira wa miguu, nyavu, kikapu, mikono, nk); michezo ya kupigana na kujilinda yaani masho ati(karate, kung fu, judo, capoeira, krav maga, jiu jitsu, systema, kickboxing, thai boxing, kempo, kalari payatu, aikido, nk)

Ni muhimu mwanadamu ufanye mazoezi makali ya viungo mara mbili tatu kwa juma. Si vizuri kufanya kila siku kwani musuli na mishipa inahitaji kupumzika na kukua.

Kama unapenda kuinua vyuma lazima uwe na mwalimu wa kukuelekeza; na si vizuri kufanya kila siku.  Wastani wa mara mbili tatu kwa juma inatosha kabisa.

 

6-UPO UFANYAJI MAZOEZI WA AINA MBILI

Mazoezi ya nguvu ya kuhema niliyotaja hapo juu (cardio-vascular) na yale laini ya kujinyoosha yaani ambayo hutumia zaidi nguvu za ndani na pumzi.

Haya ya pili ni kama Yoga (India) , Tai Chi Chuan (China) na aina mpya mazoezi iliyoanza Majuu miaka ya karibuni yaani Pilates (hutamkwa hivyo hivyo ilivyoandikwa Pilates).

Haya laini yanawafaa zaidi watu wazima na nchini China na Japan mathalan utawakuta wazee wa miaka 80 hadi 90 bado wanayafanya. Husaidia moyo, damu na akili.

Michezo na mazoezi ya mwili ni njia kuu ya kupunguza unene, kurefusha maisha, kuchangamsha ubongo, kupunguza ulevi, uvutaji sigara, dawa za kulevya, tabia mbaya za uvivu, ugomvi, nk.  Mataifa yenye watu wanaofanya mazoezi kama Japan, Brazili, India, China nk  huwa na wachapa kazi wengi na wananchi wanaoipenda jamii yao.

Chakula cha wanga kwa wingi kilichozoeleka sana Afrika ni kitamu; ila kinakosa mboga mbichi za majani, yaani Saladi

7-KULA SANA CHUMVI SI VIZURI

Ulaji chumvi mwingi hutokana na suala la ladha. Kisayansi vyakula  vyote vina chumvi asilia sema tu tumezoea kuongezea madini hii iitwayo Sodium.

Sodium inachangia sana kufupisha maisha. Huifanya mishipa ya damu ichoke; ni kama bomba lolote la maji ukilitazama baadaye hugeuka rangi kutokana na yale maji kupita pale kila siku.

Kwa wale tunaoishi nchi za joto na kutoka sana jasho kula chumvi ni muhimu. Ila tatizo letu ni kwamba hatunywi maji ya kutosha.

Mtu ukiwa na kiu unakunywa soda au kinywaji cha sukari; inakuwa kama unaendelea kuutesa mwili.

Kwa vipi? Mishipa inayopitisha damu mwilini badala ya kusaidiwa kwa maji inawekewa kazi zaidi ya kusafisha sukari na chumvi. Ndiyo maana vifo vingi vinatokea mapema; wastani wetu wa maisha haupiti miaka 50.

Utafiti uliofanywa chuo kikuu cha California, Marekani mwanzoni mwa 2010, umethitibisha kwamba vifo vingi duniani husababishwa na maradhi ya moyo na saratani ambavyo hutokana na uvutaji sigara, unene, ulevi na ulaji sana wa chumvi na sukari.
Tukipunguza ulaji wa chumvi tunasaidia pia kupunguza maradhi ya moyo, utafiti unasema.


8-TAFITI ZA VYUO KADHAA ULIMWNGUNI KUHUSIANA NA AFYA

Jarida la Kimarekani la sayansi lilieleza kwamba utapunguza ugonjwa wa moyo (ambao husababishwa na unene , wasiwasi na purukshani) kwa asilia mia 42 kama utakula matunda na mboga za majani peke yake kila siku, juu ya msosi wa kawaida.

(PENDEKEZO LA KULA- Na 4- Kula mlo wako. Baada ya saa mbili au tatu, sakatia tunda au matunda; baada ya mlo mwingine, kula sahani ya mseto wa mboga mbichi kama karote na matango. Utaona tofauti ya afya, ngozi, wajihi,usingizi, nk.

Kidesturi tumezoea kunywa chai au soda za sukari sukari na gesi kati kati nya milo badala ya matunda na mboga mbichi za majani).

Utafiti uliofanywa na wanasayansi  chuo kikuu cha South Carolina mwanzo wa mwaka 2010 kuhusu faida za kuogelea.

-Zoezi la kuogelea  lina faida zaidi ya kukimbia au kutembea kwa vile huchanganya mazoezi makali na pumzi, kusaidia mapafu na moyo. Utafiti ulithibitisha kuogelea hupunguza hatari za kifo kwa asili mia hamsini.

-Utafiti wa jarida la chuo cha uganga Ulaya umeeleza (desemba 2009) kwamba kulala nusu saa kila mchana (“nap”) husaidia  kupunguza ugonjwa wa moyo kwa asilimia 37.

-Uchunguzi wa chuo cha michezo cha Hispania mwanzoni mwa 2010 umethibitisha kwamba ukikimbia mara tatu kwa juma (jogging) unaongeza nyege mwilini kwa asili mia 75. Hasa kwa watu wa makamo mnaoanza kupoteza nguvu za urijali.

-Uchunguzi chuo kikuu cha Leeds, Uingereza  mwanzoni mwa 2010 umeonyesha unapotembea kwa miguu, ukikwepa barabara kubwa zisisokuwa na mioshi ya magari (pollution) unapunguza matatizo ya maradhi ya hewa chafu kama pumu, mapafu na appendix.

-Uchunguzi wa chuo kikuu cha Texas mwaka 2010 umegundua kwamba  kula tunda la divai nyekundu mara kwa mara husaidia kupunguza  kupata ugonjwa wa kisukari.

-Hapo hapo tunaelezwa kwamba watu weusi na bara la Asia wanakumbwa zaidi na ugonjwa wa kisukari kutokana na vinywaji vya sukari sukari na gesi (fizzy drinks).

Ukinywa kiasi cha miligramu 300 za vinywaji hivi (Cocacola, Red Bull, Fanta, nk)  kwa siku unajitahadharisha kupata kisukari.

9-KUFUNGA

Neno kufunga linatambuliwa rasmi kuhusiana na Waislamu (mwezi Ramadhani) au Wakristo (Lenti nk). Ufungaji huo una masharti mengine ya kidini tofauti na haya ya kiafya.

Mathalani wafungaji  hawa hula chakula kingi usiku; ukihesabu wanafunga wastani wa saa 12 tu. Kawaida ukitaka virusi na takataka nyingine mwilini zitoweke, au viungo vipumzike wahitaji saa 20 kuendelea.

Ufungaji ninaouongelea ni ufungaji wa kutokula kabisa kwa saa 24, 36 hadi 48 kuendelea…
Ufungaji ni nini?

Kama mashine yeyote mwili wa mwanadamu unahitaji kupumzika na kujisafisha. Hata tukiwa tumelala bado viungo mbalimbali mwilini vinafanya kazi.

Kwa hiyo faida ya kwanza kabisa ya kufunga ni kuupumzisha mwili kama mfanyakazi yeyote anapokwenda likizo.

Faida ya pili ya kufunga ni kusafisha mwili kutokana na uchafu ambao haukutoka (kinyesi hakitoi mabaki yote toka utumbo mkubwa), dawa na takataka za mazingira tunayoyavutia hewa, virusi au kuyanywa katika maji na vyakula mbalimbali na pia uchafu wa hisia, yaani hasira, huzuni, nk.

Kuna ufungaji wa aina mbalimbali.

1-Kufunga kwa kunywa maji tu, saa 24 kuendelea…
2-Kufunga kwa kutokunywa maji au kula chochote, saa 24 kuendelea…
3-Kufunga kwa kula tu matunda au mboga zilizopondwa kama karote, matango nk, saa 24 kuendelea…

Ufungaji huu unatakiwa ufanywe kwa mpangilio. Kitu muhimu si tu kufunga bali NAMNA unavyofungua.

Ukianza kula tena, unaanza taratibu. Kawaida ni vizuri kuanza na maji, kikombe au bilauri ya kwanza taratibu.

Subiri tena nusu saa, bilauri nyingine, halafu hadi ya tatu, halafu ndiyo matunda yasiyo ya chachu, na kadhalika.

Kuanza kufungua kwa kunywa chai ya maziwa, uji au vyakula vingine vya wanga hakusadii sana mfungo huu.

Maana lengo lake ni kusafisha mwili.

10-USINGAJI

Usingaji au masaji ni njia nzuri sana ya kupunguza unene. Ikiwa unaangalia namna unavyokula, unafanya mazoezi na kusingwa mara moja au mbili kwa mwezi unaupalilia mwili vizuri.

Nini faida ya usingaji? Kusinga husaidia ngozi, mishipa ya damu na sura nzima ya mwili na taswira yako mwanadamu.

Wengi wetu tunaposikia neno kusinga tunafikiria usingaji wa mapenzi. Hivi ni vitu viwili tofauti kwani usingaji wa mapenzi unaimanisha mahusiano ya kihisia.

Kifupi mwanadamu unatakiwa uwe unautunza na kuungalia mwili wako kama nyumba au hekalu lako. Wengi wetu tunaoga, tunajipaka marashi, tunasuka, tunanyoa nywele au ndevu; lakini miili yetu kiundani inaoza taratibu…

By kiwa strong...........