Wednesday 25 March 2015

Tanzania na Kenya zimetiliana saini kulinda na kutunza misitu





Katibu Mkuu wa Wizara ya Mazingira na Maliasili nchini Kenya Richard Lusiambe (wakwanza kulia) akiongozana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki nchini Tanzania Gladness Mkamba mara baada ya kutia saini makubaliano ya Tanzania na Kenya kupiga vita biashara haramu ya mbao pamoja na mazao ya misitu inayofanyika kupitia mipaka ya nchi hizo katika mkutano uliofanyika jijini Arusha.

Makubaliano hayo yamefanyika hii leo jijini Arusha mbele ya wakurugenzi na wataalamu mbalimbali wa masuala ya maliasili na misitu kutoka nchini Kenya na Tanzania katika ukumbi wa mikutano wa Naura Hotel.

Serikali ya kenya imeishukuru Tanzania kwa kusaini makubaliano hayo na kuahidi kulinda misitu ambayo imepakana na Tanzania pamoja na kukabiliana na uhalifu unaofanywa na majangili.

Akizungumza katika makubaliano hayo katibu mkuu wa wizara ya mazingira nchini Kenya Richard Lisyambe,amesema  kila mwaka zaidi ya dola 15 zinapotea kwa ajili ya kukabiliana na wawindaji haramu na wanaofanya biashara ya bidhaa zitokanazo na na misitu kinyume na sheria.

Amesema kuwa asilimia 65 ya wananchi wa Kenya wanatumia mkaa hali ambayo inachangia uharibifu wa misitu huku akieleza kuwa watahakikisha wanapunguza kwa kiasi kikubwa matumizi ya mkaa kwa kutoa elimu kwa wananchi nchini humo.

Kwa upande wake afisa misitu Tanzania Juma Mgoo amesema kuwa huu ndio muda wa wananchi kuelewa umuhimu wa mali asili na misitu na kuahidi kusimamia ipasavyo na kusema kuwa watahakikisha wanawachukulia hatua kali za kisheria kwa yeyote atakaebainika kufanya uharibifu wowote wa mazingiara.

Makubaliano haya yamekuja ikiwa nchi zote mbili Tanzania na Kenya zipo katika vita kubwa ya kukabiliana na majangili ambao wanatishia kutoweka kwa maliasili zilizopo ikiwa ni pamoja na wanyamapori.

0 comments:

Post a Comment