Mahakama nchini Ivory Coast imemhukumu aliyekuwa mke wa Rais wa nchi hiyo Laurent Gbagbo, kifungo cha miaka 20 gerezani. Simone Gbagbo amehukumiwa kifungo hicho baada ya kukutwa na hatia ya kushiriki katika ghasia zilizotokea baada ya uchaguzi nchini humo mwaka 2010 na 2011. Simone Gbagbo alikamatwa mwaka 2011 pamoja na mume wake, aliyekuwa rais wa nchi hiyo Laurent Gbagbo, ambaye anakabiliwa na mashtaka ya uhalifu dhidi ya binadamu katika mahakama ya uhalifu mjini The Hague Uholanzi. Katika ghasia hizo watu takriban elfu tatu walifariki dunia.
MAFUTA NA GESI NI NGUZO YA UCHUMI WA TAIFA
-
*Sekta ya mafuta na gesi kama nguzo ya maendeleo ya Taifa*
Na Rashid Mtagaluka.
Tarehe 14 Novemba 2025, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe....
4 hours ago







0 comments:
Post a Comment