Mahakama nchini Ivory Coast imemhukumu aliyekuwa mke wa Rais wa nchi hiyo Laurent Gbagbo, kifungo cha miaka 20 gerezani. Simone Gbagbo amehukumiwa kifungo hicho baada ya kukutwa na hatia ya kushiriki katika ghasia zilizotokea baada ya uchaguzi nchini humo mwaka 2010 na 2011. Simone Gbagbo alikamatwa mwaka 2011 pamoja na mume wake, aliyekuwa rais wa nchi hiyo Laurent Gbagbo, ambaye anakabiliwa na mashtaka ya uhalifu dhidi ya binadamu katika mahakama ya uhalifu mjini The Hague Uholanzi. Katika ghasia hizo watu takriban elfu tatu walifariki dunia.
TANZANIA,JICA KUPANUA USHIRIKIANO KWENYE UTAFITI WA MADINI MUHIMU NA
KIMKAKATI
-
-Zaidi ya Wataalamu 30 Wanufaika na mafunzo kupitia Mradi wa Kizuna
📍 Dodoma
Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Madini na Shirika la Ushirikiano wa...
4 hours ago







0 comments:
Post a Comment