Utashi wa kisiasa upo ili kukemea ukatili dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi albino,amesema Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Dk. Pindi Chana, baada ya Ofisi ya Haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa kuziomba serikali za Tanzania, Malawi na Burundi kuchukua hatua za kusitisha mauaji hayo. Bi Chana amesema hatua ya kwanza itakayochukuliwa na serikali ya Tanzania ni kuwapatia wahalifu wa mauaji hayo adhabu kali, ikiwemo hukumu ya kifo, hata kama Tanzania haijatekeleza adhabu hiyo kwa muda mrefu. Kadhalika amesema kama nchi nyingine zinzvyochukua hatua dhidi ya ugaidi, serikalia ya Tanzania ina haki ya kuchukua hatua kali dhidi ya vitendo vya mauajia ya albino. Hatimaye ametoa wito kwa watanzania wote waonyeshe ubinadamu na huruma ili kukomesha ukatili huo ambao ni kinyume na haki za binadamu.
Benki ya CRDB yakabidhi madarasa Sekondari ya Kikilo, Shule ya Msingi
Isabe, Kondoa
-
Benki ya CRDB kupitia sera yake ya uwekezaji kwa jamii, Aprili 24 - 25,
2024 ilikabidhi madarasa mawili katika Shule ya Sekondari Kikilo na
madarasa mengi...
4 hours ago
0 comments:
Post a Comment