Utashi wa kisiasa upo ili kukemea ukatili dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi albino,amesema Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Dk. Pindi Chana, baada ya Ofisi ya Haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa kuziomba serikali za Tanzania, Malawi na Burundi kuchukua hatua za kusitisha mauaji hayo. Bi Chana amesema hatua ya kwanza itakayochukuliwa na serikali ya Tanzania ni kuwapatia wahalifu wa mauaji hayo adhabu kali, ikiwemo hukumu ya kifo, hata kama Tanzania haijatekeleza adhabu hiyo kwa muda mrefu. Kadhalika amesema kama nchi nyingine zinzvyochukua hatua dhidi ya ugaidi, serikalia ya Tanzania ina haki ya kuchukua hatua kali dhidi ya vitendo vya mauajia ya albino. Hatimaye ametoa wito kwa watanzania wote waonyeshe ubinadamu na huruma ili kukomesha ukatili huo ambao ni kinyume na haki za binadamu.
Britam Tanzania Yawekeza Katika Miradi ya Maji na Upandaji Miti Kwenye
Shule Mbili za Msingi
-
Britam Insurance Limited (Tanzania) imewekeza TZS milioni 40 katika mradi
wa maji safi unaolenga shule mbili za msingi jijini Dar es Salaam, ikiwa ni
se...
1 hour ago







0 comments:
Post a Comment