Mwandishi maarufu wa runinga kutoka Afrika Kusini ameibiwa hadharani alipokuwa akijiandaa kwenda hewani mbele ya kamera. Kanda ya video imewaonyesha wanaume wawili wakimvamia Vuyo Mvoko, kutoka yuninga ya taifa ya SABC ambaye alikuwa nje ya hospitali moja ya mjini Johannesburg akiripoti kuwasili kwa rais wa Zambia ili kufanyiwa ukaguzi wa matibabu. Bwana Mvoko baadaye alisema kuwa mmoja wa wezi hao alimtishia na bunduki alipokataa kumpa simu yake ya rununu. Wezi hao walionekana kutojali kamera zilizokuwa mbele yao. ''Sikuelewa ni kwa nini waliweza kunivamia mbele ya Kamera ilihali taa zote zilikuwa zikiwaka na kamera zilikuwa zikinasa kila kitu na, waliona kilichokuwa kikiendelea''. Baada ya mda mfupi bwana Mvoko ambaye ni mhariri wa kituo hicho cha habari alituma ujumbe katika mtandao wake wa Twitter akisema kuwa yuko salama salmin na kutuma kanda ya video hiyo mtandaoni. Maafisa wa polisi wanasema kuwa wezi hao waliiba laptopu, na simu na kwamba maafisa walikuwa tayari wanachunguza kisa hicho.
Kimataifa : EU na UNHCR Wasaini makubaliano ya zaidi bilioni 9 kuimarisha
Ulinzi na msaada wa wakimbizi
-
Mwandishi Wetu , Dar Es Salaam.
Umoja wa Ulaya (EU) na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi
Duniani (UNHCR) wamesaini makubaliano mapya ya u...
2 hours ago
0 comments:
Post a Comment