Thursday 4 June 2015

Marekani yakiri kutuma kimeta zaidi…..!!



 
Maofisa wa ulinzi nchini marekani wamekiri kuwa maabara kadhaa zilizopokea kimakosa sampuli hai za vidudu hatari vya kimeta ni zaidi ya mara mbili ya matarajio ya awali.

Pentagon imesema vifaa hamsini na moja katika majimbo kumi na saba nchini Marekani, pamoja na maabara zilizopo nchini Canada, Australia na Korea kusini walitumiwa sampuli hizo kutoka maabara ya jeshi la marekani.
Imesema usafirishaji wa vijidudu hivyo vilianza miongo kadhaa iliiyopita na iliendelea mpaka wiki iliyopita.
Hadi sasa hakuna mtu aliyeathirika lakini zaidi ya watu ishirini walikuwa wakibeba sampuli hizo wamekuwa wakitibiwa kwa tahadhari tu.

0 comments:

Post a Comment