Friday 12 June 2015

Siku ya Albino kuazimishwa duniani kwa mara ya kwanza June 13-2015....

Ikiwa kesho ni maadhimisho ya kwanza kabisa ya siku ya kuhamasisha jamii kuhusu haki ya watu wenye ulemavu wa ngozi Albino, kamishna Mkuu wa haki za binadamu kwenye Umoja wa Mataifa Zeid Ra'ad Al Hussein,amesema ni fursa ya kutambua vipaji adhimu walivyo navyo kundi hilo.

Siku hiyo inaadhimishwa tarehe 13 mwezi huu kwa kutambua umuhimu wa kulinda haki za watu wenye ulemavu wa ngozi, wakati huu ambapo wanakumbwa na madhila ikiwemo kuuawa kwa imani za kishirikina.
Kamishna Zeid amesema ni lazima kutambua kuwa watoto wanaozaliwa na ulemavu wa ngozi, ni kutokana na jenetiki zilizopo kwenye familia zao,lakini ukosefu wa uelewa huwatumbukiza kwenye madhila kutokana na rangi ya ngozi yao.
Nchini Tanzania siku hii itaazimishwa mkoani Arusha,na inazaniwa kuwa huenda Arusha imepewa heshima hiyo kutokana na kutokuwa na matukio ya kuuwawa kwa Albino,ikilinganisha na mikoa mingine ya Tanzania.
Kiwale11.blogspot.com imepiga story na Vick Mtetema mkurugenzi wa shirika la Under the same Sune, ambalo linapambana na vitendo vya ukatili kwa watu wenye ulemavu wa ngozi,msikie hapa chini kwa kubonyeza play anazungumzia kuhusiana na siku hiyo ya watu wenye ulemavu wa ngozi duniani.


0 comments:

Post a Comment