Friday 19 June 2015

Chad yapiga marufuku vazi la hijabu…!!!!

Ikiwa jana waislamu katika maeneo mengi dunia wameanza mwezi mtufu wa  ramadhani,nchini chad imetolewa amri ya mtu yoyote kutovaa vazi la hijabu.

Amri hiyo inatokan na Shambulio la Kigaidi limetokea Chad Jumatatu June 15 2015 katika Jiji la N’Djamena, huku watu 23 wakiuawana na wengine zaidiya 100 wakipata majeraha makubwa.
Waziri Mkuu wa Chad Kalzeube Pahimi Deubet,amesema mtu aliyelipua mabomu hayo alitumia vazi ambalo linavaliwa na wanawake wa kiislamu ambalo linaziba mpaka usoni.

Agizo hilo limetolewa jana June 18 2015 hivyo hakuna mtu yoyote anaeruhusiwa kuvaa vazi hilo popote ndani ya Chad.


Japo haijathibitika ni nani kahusika na Shambulio hilo, stori mpaka sasa kutoka Chad zinataja sana kundi la Boko Haram kutokana na kitendo cha nchi hiyo kuisaidia Nigeria kupambana na Kundi hilo la wapiganaji.

0 comments:

Post a Comment