Monday 22 June 2015

Kuhusu vurungu alizofanyiwa Rais Jacob Zuma bungeni..!!

Rais Jacob Zuma
Tarehe 19 June mwaka huu Bunge la South Africa liliingia kwenye headlines katika vyombo vya habari pamoja na mitandao ya kijamii baada ya baadhi ya viongozi kutoka chama cha upinzani kuanzisha vurugu zilizo pelekea kuairishwa kwa Bunge hilo siku ya ijumaa.

Bunge tukufu la South Africa liliingia vurungu baada ya wanachama wa Economic Freedom Fighters kumzuia rais Jacob Zuma kuendelea kutoa ripoti aliokusudia kuwasilisha mbele ya bunge hilo kwa kumshambilia  rais huyo na maswali yanayohsu uwajibikaji wake, maswali ambayo yaliongaishwa na malalamiko ya yeye kukiuka katiba ya nchi hiyo, kitendo kilichopelekea rais huyo kutokupewa nafasi ya kujieleza.
Kitendo hichi kilimlazimu spika wa bunge Baleka Mbete kuairisha Bunge hilo na kuita kikao cha dharula na vyama hivyo nje ya bunge hilo baada ya vurungu kutapakaa bungeni hapo, na alipohojiwa na vyombo vya habari, Spika wa bunge la South Africa alisema amesikitishwa na kitendo hiki kufanyika na baadhi ya watu wanaotazamwa na jamii kama viongozi, na kuongezea kua, kitendo hichi sio mara ya kwanza kutokea kwani kitu kama hiki kilishawahi kutokea mwezi Agosti tarehe 21 mwaka jana ambako pia alilazimika kuairisha bunge hilo kutokana na vurungu kuanzishwa na vyama vya upinzani.
Bunge la South Africa limepinga baadhi ya malalamiko kutoka kwa viongozi wa vyama vya upinzani kua rais Jacob Zuma anakiuka katiba na kuepuka uwajibikaji na kusema kua rais huyo anategema kuonekana tena bungeni mwezi Agosti mwaka huu kwa ajili ya kutoa ripoti hio kama sheria ya nchi inavyomtaka kufanya hivyo mara nne kwa mwaka na mara moja kwa mwaka katika Baraza la taifa la majimbo.


0 comments:

Post a Comment