Monday 22 June 2015

Waendesha boda boda hatarini kuwa wagumba…!!!

Madereva wa kiume wa pikipiki maarufu kama bodaboda na wengine wanaotumia usafiri huo kwa muda mrefu wapo katika hatari ya kuwa wagumba.

Tafiti nyingine zilizofanywa zinazonyesha kuwa huenda wakakabiliwa na uhaba wa mbegu za kiume na hatimaye kushindwa kutoa mbegu za kiume zenye uwezo wa kutunga mimba.
Hali hiyo inatokana na sehemu za siri zinazozalisha mbegu,muda mwingi kuwa katika hali ya joto kitu ambacho kitaalamu kimebainisha kuwa kinafanya mishipa ya damu kutofanya vyema na kuchochea uzalishaji mbegu hizo.
Maelfu ya vijana nchini wamejiajiri kupitia usafiri wa bodaboda, huku wengi wakiwa katika umri mdogo wa kati ya miaka 18 hadi 50, kutokana na tafiti hizo huenda Tanzania ikaathirika zaidi kwa kuwa na vijana wengi wanaoweza kuwa wagumba.

Utafiti unaonyesha kuwa vijana wengi wanaokaa katika kiti cha pikipiki hupambana na joto,kutokana na ngozi laini iliyopo katika korodani,mirija ya damu hushindwa kupitisha virutubisho kutokana na msuguano mkali uliopo.

0 comments:

Post a Comment