Tuesday, 16 February 2016

RAS LION AMLILIA JOHN WOKA...

Msanii wa muziki wa kizazi kipya John Woka toka kundi la watukutu, amefariki dunia alfajiri ya february 16 katika hospitali ya Muhimbili jijini Dar es salaam.


John woka alitamba na ngoma zake kali kama mganga, hii kitu hii na kupendwa na mashabiki kwa style yake ya kurap kama mlevi.

John woka amefariki baada ya kupata ajali wakati anatengeneza gari maeneo ya sinza katika mfumo wa Ac.

Inasemekana kuna kitu kilivyetuka baada ya kufungua Ac na kumpiga kwenye paji la uso na kuingia kama nchi 3 au 2 na kusababisha damu nyingi kumwagia ndani ya kichwa.

Mpaka alipofikishwa hospitali ya muhimbili Woka alikuwa katika chumba cha ICU, na hali yake ilikuwa mbaya mpaka alipoaga dunia alfajiri ya tarehe 16 february 2016.

Bonyeza Play hapa chini kumsika kile ambacho amekizungumza Ras Lion ambaye alikuwa mtu wa karibu kabisa na John woka.

Related Posts:

  • Pombe kidogo pia yaweza kuleta saratani……….. Unywaji kidogo wa pombe hadi chupa moja kwa siku kwa wanawake na chupa mbili kwa wanaume, unaweza kusababisha hatari ya kupata saratani kulingana na watafiti. Makala moja ya Uingereza ilichambua utafiti mkubwa kutoka nch… Read More
  • Marufuku kupeana mikono Dar… Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadik, amewataka wakazi wa jijini hilo kuchukua hadhari za kiafya ikiwamo kuacha kusalimiana kwa kushikana mikono kutokana na mlipuko wa kipindupindu ambao mpaka sasa umeshawapata wa… Read More
  • Usikose nakala yako ya gazeti la TABIBU kesho alhamisi kwa bei ya sh. 500/= tu.                                         … Read More
  • Kufanya kazi kwa saa nyingi ni hatari…… Utafiti uliofanywa kwa zaidi ya watu laki tano, umeeleza kuwa watu wanaofanya kazi kwa saa nyingi, wako hatarini kupata kiharusi. Takwimu zilizochapishwa kwenye jarida la kitabibu la Lancet, linaonyesha upo uwezekano wa … Read More
  • Juma Kaseja ajiunga na Mbeya City…… Baada ya kuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu bila timu, golikipa mkongwe na mahiri Juma Kaseja August 19 amesaini mkataba wa miezi sita wa kuitumikia klabu yaMbeya City kutoka Jijini Mbeya. Mkataba wa … Read More

0 comments:

Post a Comment