Tuesday, 16 February 2016

HOSPITALI YATUMIA MAJI YA CHUPA CHUMBA CHA UPASUAJI..!!

Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala inalazimika kununua maji ya chupa,
kwa ajili ya kusafisha vifaa vya upasuaji baada ya mashine mbili za kuchujia maji kuharibika.
Hayo yamesema jana na katibu wa afya wa hospitali hiyo Willborada Athanas,wakati akipokea mashine moja ya kuchujia maji iliyotolewa na kampuni ya Tanzania Water Equipment Supply Company ( Twesco).
Amesema kwa kipindi cha miezi mitatu sasa hospitali hiyo inalazimika kununua maji kwa ajili ya kusafishia vifaa vya upasuaji, licha ya mashine moja kuuzwa Sh5.6 milioni.
Ameongeza kuwa kila baada ya wiki mbili wanalazimika kununua lita 60 za majisafi ambazo ni sawa na Sh 52,000, kwa ajili ya kusafishia vifaa.
Amesema mashine ya kwanza iliharibika miezi sita iliyopita na mtaalamu alipopelekwa kwa ajili ya kutengeneza, aligundua kuwa imeharibika na haifai kutengenezwa huku mashine ya pili ikiharibika miezi mitatu iliyopita na hivyo kusababisha changamoto kubwa katika kitengo cha upasuaji.
Amesema licha ya hospitali hiyo kupandishwa hadhi na kuwa ya rufaa, bado mfumo wa majitaka haukidhi mahitaji.

Mkurugenzi wa Ufundi wa Twesco Victor Manyanga amesema kuwa, mashine waliyokabidhi ina uwezo wa kusafisha lita 300 za maji kwa siku.

Related Posts:

  • Chachu ya kutuliza maumivu yapatikana…… Wanasayansi nchini Marekani wamesema kuwa, wamefanikiwa kutengeneza chachu yenye vina saba vinavyoweza kupunguza maumivu kwa kiasi kikubwa. Chachu hiyo inaweza kubadilisha sukari kuwa hydrocodone, dawa inayofanana na mor… Read More
  • Mtoto apata mtoto Paraguay…!!!! Binti wa miaka kumi na mmoja nchini Paraguay aliyedai kubakwa na baba yake wa kambo, amejifungua mtoto wa kike baada ya mamlaka nchini humo kumzuia asitoe ujauzito aliokua nao. Madaktari katika mji mkuu wa Asuncion wames… Read More
  • Joto kali layeyusha gari Italy………….. Siku za hivi karibuni baadhi ya maeneo Stori za joto kuongezeka,zimekuwa zikichukua nafasi kubwa sana, nikukumbushe tu kwamba ilianza kule Dubai ambapo  joto lilipanda mpaka kufikia nyuzi 38, tukasikia … Read More
  • Sasa unaweza kununua gazeti lako pedwa la afya Tanzania kwa sh. 300/= tu kwenye app ya mPaper inayopatikana kwenye google play store. … Read More
  • Google yajiimarisha kupitia Alphabet... Katika hatua yake ya kujiimarisha zaidi Google itaendelea kusimamia biashara zake kama vile programu,You Tube na Android. Lakini idara zake mpya kama vile ile ya uwekezaji pamoja na utafiti ,smart-home',unit test na d… Read More

0 comments:

Post a Comment