Tuesday 16 February 2016

HOSPITALI YATUMIA MAJI YA CHUPA CHUMBA CHA UPASUAJI..!!

Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala inalazimika kununua maji ya chupa,
kwa ajili ya kusafisha vifaa vya upasuaji baada ya mashine mbili za kuchujia maji kuharibika.
Hayo yamesema jana na katibu wa afya wa hospitali hiyo Willborada Athanas,wakati akipokea mashine moja ya kuchujia maji iliyotolewa na kampuni ya Tanzania Water Equipment Supply Company ( Twesco).
Amesema kwa kipindi cha miezi mitatu sasa hospitali hiyo inalazimika kununua maji kwa ajili ya kusafishia vifaa vya upasuaji, licha ya mashine moja kuuzwa Sh5.6 milioni.
Ameongeza kuwa kila baada ya wiki mbili wanalazimika kununua lita 60 za majisafi ambazo ni sawa na Sh 52,000, kwa ajili ya kusafishia vifaa.
Amesema mashine ya kwanza iliharibika miezi sita iliyopita na mtaalamu alipopelekwa kwa ajili ya kutengeneza, aligundua kuwa imeharibika na haifai kutengenezwa huku mashine ya pili ikiharibika miezi mitatu iliyopita na hivyo kusababisha changamoto kubwa katika kitengo cha upasuaji.
Amesema licha ya hospitali hiyo kupandishwa hadhi na kuwa ya rufaa, bado mfumo wa majitaka haukidhi mahitaji.

Mkurugenzi wa Ufundi wa Twesco Victor Manyanga amesema kuwa, mashine waliyokabidhi ina uwezo wa kusafisha lita 300 za maji kwa siku.

0 comments:

Post a Comment