Monday 1 February 2016

MWANAMKE ALIYEMUUA MUMEWE ASAMEHEWA…!!!

Rais wa Ufaransa Francois Hollande amemsamehe mwanamke aliyekuwa amefungwa jela miaka 10, kwa makosa ya kumuua mumewe kwa kumpiga risasi tatu.

Mume wa Jacqueline Sauvage alikuwa mlevi aliyezoea kumpiga, na alikuwa amembaka yeye na mabinti zake kwa miaka mingi.
Jacqueline amesema mumewe huyo pia alimnyanyasa mtoto wao wa kiume, ambaye baadaye alijiua.
Watu zaidi ya laki 4 walikuwa wametia saini ombi la kumtaka Bw Hollande, amwachilie huru mwana mama huyo.
Mawakili wa Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 68, wamesema anatazamiwa kuondoka gerezaji katikati mwa mwezi Aprili.
Siku ya tarehe 10 Septemba 2010 siku ambayo mwanawe alijiua kutokana na manyanyaso ya baba yake, mwana mama huyo alimpiga risasi mumewe mara tatu akitumia bunduki.
Alipatikana na hatia na kufungwa jela miaka 10 gerezani Oktoba 2014, na kifungo chake kikatizamwa upya Desemba 2015, baada ya rufaa yake ya kujitetea akisema kwamba alikuwa anajikinga kukataliwa.
Kesi hiyo ilifuatailiwa sana nchini humo,wengi wakitaka haki ya kutumia sababu ya kujikinga kujitetea iwekwe wazi zaidi.
Walitaka watu walionyanyaswa na kudhulumiwa nyumbani, waruhusiwe kutumia haki hiyo kujitetea.

Bw Hollande amefanya uamuzi wake siku mbili, baada ya kukutana na mabinti watatu wa mwana mama huyo.

0 comments:

Post a Comment