Wednesday, 17 February 2016

PASPOTI ZA KIELEKTRONIKI KUZINDULIWA AFRIKA MASHARIKI…

Raia wa Nchi za Afrika Mashariki wataanza kutumia paspoti za kielektroniki ambazo zitatumika kurahisisha usafiri kwa wananchi wa eneo hilo.

Hayo yamedokezwa na Mkuu wa awasiliano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki EAC Owora Richard Othieno ambaye ameongeza kuwa, kuanzia mwezi Machi, raia wa nchi za Afrika Mashariki wanaweza kupata pasi za kusafiria za kielektroniki za jumuiya hiyo ya kiuchumi, ili kusahilisha usafiri katika nchi hizo.
Owora Othieno amedokeza hayo kabla ya mkutano wa 17 wa viongozi wa nchi za EAC unaopangwa kufanyika tarehe 29 mwezi huu huko Arusha, Tanzania. Amesema, viongozi wa kanda hiyo watazindua pasi hiyo, ambayo itakuwa moja ya hatua muhimu katika kufikia lengo la kuimarisha ushirikiano wa kikanda.
Wananchi wa Afrika Mashariki wamekuwa wakisubiri pasi hiyo kwa muda mrefu na hivyo kuzinduliwa kwake ni hatua muhimu katika kuimarisha ushirikiano wa nchi tano wanachama ambazo ni Burundi, Kenya, Rwanda, Tanzania na Uganda.

Katika kikao cha mwezi huu, wakuu wa EAC watajadili ombi la Somalia kutaka kujiunga na jumuiya hiyo.

Related Posts:

  • Joto kali layeyusha gari Italy………….. Siku za hivi karibuni baadhi ya maeneo Stori za joto kuongezeka,zimekuwa zikichukua nafasi kubwa sana, nikukumbushe tu kwamba ilianza kule Dubai ambapo  joto lilipanda mpaka kufikia nyuzi 38, tukasikia … Read More
  • Japan yakumbuka shambulio la Hiroshima… Raia wa Japan leo wanaadhimisha kumbukumbu ya miaka 70 tangu shambulio la kwanza la bomu la Atomiki kutekelezwa mjini Hiroshima. Takriban watu laki moja na arobaini walikadiriwa kupoteza maisha baada ya Ndege ya Marekani… Read More
  • Google yajiimarisha kupitia Alphabet... Katika hatua yake ya kujiimarisha zaidi Google itaendelea kusimamia biashara zake kama vile programu,You Tube na Android. Lakini idara zake mpya kama vile ile ya uwekezaji pamoja na utafiti ,smart-home',unit test na d… Read More
  • Utamaduni wa kurejesha mahari marufuku Uganda…… Ngombe hutumiwa sana kulipa mahari UgandaMahakama ya juu zaidi nchini Uganda imesema kuwa utamaduni wa kurejesha mahari baadaya talaka katika ndoa za kitamaduni unakiuka katiba na utamaduni huo unapaswa kupigwa marufuku. … Read More
  • Michuano ya dunia Mpira wa pete kuanza…. Michuano ya kumi na nne ya Kombe la dunia la mchezo wa pete itaanza kutimua vumbi leo katika jiji la Sydney nchini Australia. Jumla ya michezo sitini na minne itacheza katika siku kumi za michuano hiyo ambapo timu kumi n… Read More

0 comments:

Post a Comment