Wednesday 17 February 2016

PASPOTI ZA KIELEKTRONIKI KUZINDULIWA AFRIKA MASHARIKI…

Raia wa Nchi za Afrika Mashariki wataanza kutumia paspoti za kielektroniki ambazo zitatumika kurahisisha usafiri kwa wananchi wa eneo hilo.

Hayo yamedokezwa na Mkuu wa awasiliano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki EAC Owora Richard Othieno ambaye ameongeza kuwa, kuanzia mwezi Machi, raia wa nchi za Afrika Mashariki wanaweza kupata pasi za kusafiria za kielektroniki za jumuiya hiyo ya kiuchumi, ili kusahilisha usafiri katika nchi hizo.
Owora Othieno amedokeza hayo kabla ya mkutano wa 17 wa viongozi wa nchi za EAC unaopangwa kufanyika tarehe 29 mwezi huu huko Arusha, Tanzania. Amesema, viongozi wa kanda hiyo watazindua pasi hiyo, ambayo itakuwa moja ya hatua muhimu katika kufikia lengo la kuimarisha ushirikiano wa kikanda.
Wananchi wa Afrika Mashariki wamekuwa wakisubiri pasi hiyo kwa muda mrefu na hivyo kuzinduliwa kwake ni hatua muhimu katika kuimarisha ushirikiano wa nchi tano wanachama ambazo ni Burundi, Kenya, Rwanda, Tanzania na Uganda.

Katika kikao cha mwezi huu, wakuu wa EAC watajadili ombi la Somalia kutaka kujiunga na jumuiya hiyo.

0 comments:

Post a Comment