Thursday 11 February 2016

MADUKA YAFUNGIWA KWA KUUZA KADI ZA KLINIKI…!!

Halmashauri ya Tunduma Mkoa wa Songwe, imeyafungia maduka
manne yanayotuhumiwa kuuza kadi za kliniki zenye maneno yaliyoandikwa ‘haziuzwi’.
Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Halima Mpita, amesema kuwa wameyafunga maduka hayo baada ya kuwapo kwa malalamiko kutoka kwa wananchi, juu ya watumishi wa Kituo cha Afya cha Tunduma kuwaamuru wanunue kadi hizo kinyume na sheria kwa watu binafsi, wakati zinapaswa kutolewa bure kwenye vituo vya afya, zahanati na hospitali.
Mpita amesema baada ya kupata malalamiko hayo, alituma timu ya wakaguzi kwenda kwenye maduka hayo yaliyo jirani na kituo hicho kubaini kufanyika kwa biashara hiyo haramu.
Mkurugenzi huyo ameutaka uongozi wa halmashauri hiyo, kuendelea kufuatilia huduma za afya katika zahanati zinazozunguka mji huo.     
Awali wananchi walilalamika kuuziwa kadi moja kwa Shilingi elfu 2, wakati zinapaswa kutolewa bure kwa wajawazito.

Mkazi wa Mtaa wa Sogea Farida Sichone, amesema kwa muda mrefu wamekuwa wakilazimishwa kununua kadi hizo.

0 comments:

Post a Comment