Monday 8 February 2016

MAREKANI INADAIWA ZAIDI YA TRILION 15..!!

Madeni yanayoizunguka serikali ya Marekani yanakaribia dola
trilioni 20, na kuna hofu ya kuongezeka zaidi madeni hayo.

Kwa mujibu wa takwimu rasmi ni kwamba Washington inadaiwa dola trilioni 19.8, kiasi ambacho ni sawa na asilimia 103 ya pato jumla la taifa.

Inatazamiwa kuwa kufikia mwaka 2017 wakati kama huu, madeni ya Marekani yatapanda na kufikia dola trilioni 20.

Kufuatia takwimu hizo Marekani kwa sasa inahesabiwa kuwa nchi yenye madeni mengi zaidi duniani.

Suala hilo ni kinyume kabisa na mtazamo wa watu wengi ambao hudhani kuwa Marekani ni nchi tajiri na isiyoweza kukopa.

Serikali ya Washington imekopa dola trilioni 13.7 kutoka kwa mashirika na watu binafsi na vilevile ikakopa dola trilioni 5.3 kutoka kwa hazina ya taifa.


Duru zinaarifu kuwa tangu kuanza kupindi cha uongozi wa Rais Barack Obama, madeni ya Marekani yameongezeka maradufu.

0 comments:

Post a Comment