Friday 12 February 2016

UTAFITI: WASIOFANYA ZOEZI HUZEEKA HARAKA..!!

Ukosefu wa mazoezi kwa wale walio na umri wa kadri, huzeesha akili na mwili utafiti umesema.

Ukosefu wa mazoezi kwa watu walio na umri wa miaka 40, uhusishwa na ubongo wenye ukubwa wa size 60 kulingana na utafiti nchini Marekani.
Mazoezi miongoni mwa watu wenye umri wa kadri, ni muhimu hususan kwa watu wenye ishara za mapema za ugonjwa wa moyo, wamesema watafiti katika chuo kikuu cha Boston.
Utafiti huo pia umeongezea ukuaji wa ushahidi kwamba, afya ya moyo huathiri afya ya ubongo katika maisha ya mbeleni.
Utafiti huo uliochapishwa katika jarida la matibabu katika chuo cha navu nchini Marekani, uliwahoji watu elfu 1 mia 5 na 83 walio na miaka 40.
Walioshiriki ambao hawakuwa na tatizo la akili ama hata ugonjwa wa moyo, walijipima katika mashine ya kukimbia na kufanya hivyo tena, baada ya miongo miwili pamoja na ukaguzi wa Ubongo

0 comments:

Post a Comment