Tuesday, 9 February 2016

MWINGEREZA AUZA HEWA SAFI UCHINA..!!

Maeneo mengi ya Uchina hasa miji mikubwa, yamekuwa yakitatizwa na uchafuzi wa hewa.

Hili limekuwa faraja kwa Mwingereza mmoja ambaye ameanza kuuza hewa safi huko.
Leo De Watts 27 hutoa hewa yake maeneo ya mashambani Uingereza, ambayo hayajachafuliwa na kuipakia kwenye chupa na kuisafirisha hadi miji ya Shanghai na Beijing, na kuwauzia matajiri hewa hiyo.
Chupa moja ya hewa hiyo safi ya mililita 580 huwa anauza £80 ($115).
Kutokana an biashara hiyo ameanzisha kampuni kwa jina Aethaer, na hutoa hewa yake maeneo yenye upepo mwingi ya Dorset, Somerset, na Wales.
Anasema baadhi ya wateja hutaka hewa ya kiwango Fulani, na wakati mwingine humbidi kutoa hewa maeneo ya milima, na wakati mwingine bondeni ili kupata aina ya hewa inayohitajika na wateja wake.
Linaonekana kama wazo la kushangaza sana hapa kwetu sababu tuna hewa safi, lakini huko kwawenzetu hakuna hewa safi na inathaminiwa sana.

Viwango vya uchafuzi wa hewa Uchina vilifikia viwango vya juu sana, hasa mwezi Desemba, na katika baadhi ya maeneo kusababisha shule kufungwa.

Lakini Watts si mtu wa kwanza kuuza hewa nchini China, kwani kunao wafanya biashara ambao wamekuwa wakiuza hewa safi kutoka nchini kama vile Canada.

Related Posts:

  • 'Viagra' ya wanawake yazinduliwa Marekani………. Shirika la Dawa na Chakula nchini Marekani (FDA) limeidhinisha matumizi ya dawa ya kwanza kabisa iliyoundwa mahususi kuwatibu wanawake ambao hawana hamu ya kufanya mapenzi maarufu ''viagra ya wanawake'' Dawa hiyo inavi… Read More
  • Pistorious kuachiliwa Ijumaa Mwanariadha mshindi wa nishani ya dhahabu ya Olimpiki katika raidha Oscar Pistorius ataachiliwa kutoka gerezani ijumaa wiki hii.Mwanariadha huyo raia wa Afrika Kusini alihukumiwa kifungo cha miaka mitano gerezani mwaka ulio… Read More
  • Juma Kaseja ajiunga na Mbeya City…… Baada ya kuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu bila timu, golikipa mkongwe na mahiri Juma Kaseja August 19 amesaini mkataba wa miezi sita wa kuitumikia klabu yaMbeya City kutoka Jijini Mbeya. Mkataba wa … Read More
  • Usikose kusoma gazeti la TABIBU kesho alhamisi likiwa limesheheni habari mbalimbali kuhusu afya. Ni kwa bei ya sh. 500/= !!                             … Read More
  • Pombe kidogo pia yaweza kuleta saratani……….. Unywaji kidogo wa pombe hadi chupa moja kwa siku kwa wanawake na chupa mbili kwa wanaume, unaweza kusababisha hatari ya kupata saratani kulingana na watafiti. Makala moja ya Uingereza ilichambua utafiti mkubwa kutoka nch… Read More

0 comments:

Post a Comment