Tuesday 9 February 2016

MWINGEREZA AUZA HEWA SAFI UCHINA..!!

Maeneo mengi ya Uchina hasa miji mikubwa, yamekuwa yakitatizwa na uchafuzi wa hewa.

Hili limekuwa faraja kwa Mwingereza mmoja ambaye ameanza kuuza hewa safi huko.
Leo De Watts 27 hutoa hewa yake maeneo ya mashambani Uingereza, ambayo hayajachafuliwa na kuipakia kwenye chupa na kuisafirisha hadi miji ya Shanghai na Beijing, na kuwauzia matajiri hewa hiyo.
Chupa moja ya hewa hiyo safi ya mililita 580 huwa anauza £80 ($115).
Kutokana an biashara hiyo ameanzisha kampuni kwa jina Aethaer, na hutoa hewa yake maeneo yenye upepo mwingi ya Dorset, Somerset, na Wales.
Anasema baadhi ya wateja hutaka hewa ya kiwango Fulani, na wakati mwingine humbidi kutoa hewa maeneo ya milima, na wakati mwingine bondeni ili kupata aina ya hewa inayohitajika na wateja wake.
Linaonekana kama wazo la kushangaza sana hapa kwetu sababu tuna hewa safi, lakini huko kwawenzetu hakuna hewa safi na inathaminiwa sana.

Viwango vya uchafuzi wa hewa Uchina vilifikia viwango vya juu sana, hasa mwezi Desemba, na katika baadhi ya maeneo kusababisha shule kufungwa.

Lakini Watts si mtu wa kwanza kuuza hewa nchini China, kwani kunao wafanya biashara ambao wamekuwa wakiuza hewa safi kutoka nchini kama vile Canada.

0 comments:

Post a Comment