Monday, 22 February 2016

RIPOTI: KINONDONI KINARA WA UHALIFU….!!


Ripoti ya awali ya Utoaji wa Huduma za Kipolisi (PDB) inayosimamia usalama wa raia na
mali zao, inaonyesha Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni unaongoza kwa vitendo vya uhalifu.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa ripoti hiyo tarehe 18 feb 2016 jijini Dar es Salaam Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Ernest Mangu, alisema ripoti hiyo imetolewa ili kupanga mikakati mipya ya kupambana na vitendo vya uhalifu katika maeneo mbalimbali ya nchi ikiwamo Kinondoni.
Alisema kutokana na hali hiyo, jeshi hilo limejipanga kuhakikisha vitendo hivyo vinakwisha ili wananchi waishi kwa amani na utulivu.
Aliongeza kuwa hadi sasa wamefungua vituo vya kanda za kipolisi 37 maeneo mbalimbali ya mkoa huo ambavyo vitakuwa na askari wa kutosha, ambao watakuwa na silaha kwa ajili ya kufanya doria.
Alisema askari hao watakuwa tayari kupambana na uhalifu wa aina yoyote utakaojitokeza.
Mangu alisema ripoti hiyo imetolewa chini ya Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN) ambao unahitaji kutekelezwa kwa vitendo.
Aliwataka askari wa jeshi hilo kila mmoja kutimiza majukumu yake kulingana na nafasi yake ili waweze kupambana na uhalifu.

Alisema endapo Serikali itatoa fedha za kutosha, kazi hiyo itaendelea katika mikoa mingine ya kipolisi ya Ilala na Temeke na baadae kusambaa nchi nzima.

Related Posts:

  • Raia Nigeria wapinga posho za wabunge…!!! Wananchi wa Nigeria wamechukizwa na taarifa kwamba wabunge wamejiidhinishia mamilioni ya dola kwa ajili ya posho ikiwemo ya mavazi. Gazeti moja nchini Nigeria limesema kuwa kwa mujibu wa sheria ya posho inayohusisha pi… Read More
  • Askofu kushtakiwa kwa kudhulumu watoto…!!! Askofu Josef Weslowski kushtakiwa kwa kudhulumu watoto Kiongozi wa kanisa katoliki duniani Papa Francis, ameonekana kuanza kuwakabili makasisi waliotuhumiwa kwa sakata ya ngono. Askofu mmoja aliyekua mjumbe wa papa katik… Read More
  • China yaipa Takukuru vifaa vya bilioni 3…. Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Dk. Edward Hoseah. Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China, imeikabidhi Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) vifaa vya kiufundi vya Sh. bilioni tatu, kwa ajili ya kuiongezea ufanis… Read More
  • Unafahamu kwa nini kuna siku ya mtoto wa Africa…!!! Tarehe 16 Juni ya kila mwaka Tanzania huungana na Nchi nyingine za Afrika kuadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika. Mnamo mwaka 1990 uliokuwa Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU),ulipitisha Azimio la kuwakumbuka watoto wa ki… Read More
  • Kiongozi wa Al Qaeda nchini Yemen auawa…!! Kiongozi wa Al Qaeda nchini Yemen auawaTawi la kundi la Al Qaeda nchini Yemen limethibitisha kuuawa kwa kiongozi wake wakati wa shambulizi la ndege isiyokuwa na rubani ya Marekani.Ripoti kutoka kwa maafisa wa usalama nchini… Read More

0 comments:

Post a Comment