Wednesday, 17 February 2016

MKENYA MIONGONI MWA WALIMU BORA DUNIANI..!!

Mwalimu mmoja kutoka Kenya ni miongoni mwa walimu wengine kumi waliofuzu fainali ya
waliorodheshwa, kuwania tuzo ya mwalimu bora katika harakati zake za kukabiliana na itikadi kali.

Ayub Mohammed ni mwalimu wa somo la biashara na lile la dini la IRE, katika shule ya upili ya Eastleigh mjini Nairobi.
Tuzo hiyo ya dunia ilioanzishwa na hazina ya fedha ya Verkey, ikiwa ni shirika la hisani la kampuni ya kimataifa ya elimu ya Gems, inayolenga kutafuta habari za mashujaa wanaobadilisha maisha ya vijana.
Amekuwa akijenga mtandao wa walimu walio na maono kama yake, na kutengeza utaratibu unaolenga kukabiliana na itikadi kali.
Tuzo hiyo ilipata maombi kutoka kwa walimu katika mataifa 148.
Mshindi ambaye atatangazwa mwezi Machi atapokea dola milioni moja.
Walioorodheshwa ni pamoja na Aqeela Asifi ambaye anawafunza wakimbizi nchini Pakistan na Hana Al Hroub, ambaye alilelewa katika kambi moja ya wakimbzi nchini Palestina na ambaye sasa ni mwalimu.
Mshindi wa tuzo hiyo mwaka jana alikuwa Ancie Atwell kutoka Marekani, ambaye alitoa fedha hizo kwa shule yake.
Tuzo hizo zilitolewa katika sherehe iliohudhuriwa na aliyekuwa rais wa Marekani Bill Clinton huku Bill Gates akitoa mchango wake.

Related Posts:

  • MITSUBISHI YAKIRI MAKOSA KWA MAGARI YAKE… Kampuni ya kuunda magari ya Japan ya Mitsubishi, imekiri kufanya makosa kwa tamwimu za matumizi ya mafuta kwa zaidi ya magari 600,000. Mauzo ya hisa za kampuni hiyo yalifunga yakiwa yameshuka kwa asilimia 15 kutokana na… Read More
  • WAFANYAKAZI WA RADIO 5 WAPIGWA MSASA NA BBC MEDIA ACTION.... Wafanyakazi wa Radio 5 jijini A rusha wamepatiwa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kitaaluma ili waweze kuandika habari za kuboresha maisha ya jamii kwa kupata maendeleo kuelekea uchaguzi mkuu,mafunzo hayo yanaendeshwa na sh… Read More
  • Zijue faida za ajabu za kula karanga..! Wengi wetu huchukulia ulaji wa karanga kama chakula cha kujiburudisha na kisichokuwa na umuhimu sana katika afya ya mwili wa binadamu. Kiukweli karanga siyo chakula cha kupuuziwa iwapo utajua faida zake kama nitakavyokujuza… Read More
  • VOLKSWAGEN KUNUNUA MAGARI YAKE..! Kampuni ya magari ya Volkswagen, imetangaza kuyanunua magari ya kampuni yake kutoka kwa wateja nchini Marekani yapatayo nusu milioni. Hii ni kama sehemu ya kutimiza makubaliano yaliyofikiwa na idara ya sheria ya Marek… Read More
  • MALKIA ELIZABETH ATIMIZA MIAKA 90… Siku ya leo tarehe 21-4-2016 Malkia Elizabeth ametimiza miaka tisini ya kuzaliwa. Malkia atasheherekea siku hii kwa kukutana na wananchi wake katika matembezi atayafanya huko Windsor. Malkia Elizabeth ametawala kwa mu… Read More

0 comments:

Post a Comment