Monday, 22 February 2016

SAMSUNG YAZINDUA SIMU MPYA YA GALAXY S7…

Kampuni ya kutengeneza simu ya Samsung imezindua simu yake mpya ya kisasa aina ya Galaxy S7
na Galaxy S7 Edge.
Kampuni hiyo ya kutokea Korea Kusini imezindua simu hizo mbili, ilikukabiliana na upinzani mkali kutoka kwa kampuni ya simu ya Apple.
Simu hizo za Galaxy S7 zimerejeshewa uwezo wa kusoma kadi ya kuhifadhia data al maarufu (MicroSD card)
Kikubwa kitenolojia katika simu hizo mpya za Galaxy S7 ni kuwa zinaweza kutumika hata ndani ya maji bila ya kuharibika.
Vile vile Galaxy S7 zina programmu iliyoimarishwa zaidi mbali na kuwa na kamera ya nyuma yenye uwezo wa kupiga picha hata kwenye mazingira yenye giza totoro na picha hizo zikaonekana bora.
Wadadisi wa maswala ya teknolojia hata hivyo hawaoni tofauti kubwa kimsingi kati ya simu hiyo ya Galaxy S7 na ile ya awali ya Galaxy S6.
Hilo ndilo litakalowasumbua wauzaji wa simu hiyo mpya kwani umbo na ukubwa wake ni sawasawa na ile ya Galaxy S6.
Samsung huwa haitangazi idadio ya simu ilizouza.
Hata hivyo idadi ya mauzo ya kampuni hiyo ilizorota kwa asilimia 2% katika mwaka wa 2015.
Wapinzani wake wakuu Apple, Huawei na Xiaomi hata hivyo walisajili kuimarika kwa faida zaidi.
Takwimu ya kampuni moja ya mauzo ya teknolojia IDC inaonesha kuwa kampuni hiyo ya Korea Kusini ni bora zaidi katika mauzo ya simu katika vitengo tofauti kote duniani.
Simu hiyo mpya ya Galaxy S7 inaurefu wa nchi 5.5in (14cm).

Simu ya awali ya Galaxy S6 inaurefu wa nchi 5.1 (13cm)

Related Posts:

  • TMA YATOA TAHADHARI KWA WANANCHI……. Mamlaka ya hali ya hewa iliyopo chini ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano nchini Tanzania imewatahadharisha wananchi kuwepo kwa hali mbaya ya hewa katika maeneo yote ya pwani kuanzia leo usiku. Hayo yamebaini… Read More
  • WATU WAPIGA KURA UCHAGUZI MKUU ITALIA… Watu nchini Italia wanapiga kura baada ya kampeni zilizoangazia zaidi masuala la uhamiaji na uchumi. Waandishi wa habari wanasema kuwa ni vigumu kusema ni nani atashinda katika kura hiyo. Upande wa Five Star Movement, … Read More
  • INSPEKTA WA POLISI NA WAZIRI WA ULINZI WAFUKUZWA KAZI… Rais wa Uganda Yoweri Museveni, amemfuta kazi Inspekta mkuu wa polisi Kale Kayihura na waziri wa Ulinzi Henry Tumukunde. Generali Kayihura ambaye ni mkereketwa wa vita vilivyomsaidia rais Museveni kuingia madarakani mwa… Read More
  • VIDEO: MOTO WATEKETEZA SOKO LA MBAGALA…. Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu–Dar, asubuhi ya leo Machi 6, 2018. Sehemu iliyoathirika zaidi ni ya wauza mitumba huku baadhi ya bi… Read More
  • MWANAMUME AJIPIGA RISASI NA KUJIUA NJE YA WHITE HOUSE…. Mwanamume mmoja amejipiga risasi na kujiua nje ya Ikulu ya Marekani ya White House mjini Washington, kikosi cha kumlinda rais kimesema. Kikosi hicho kilisema kuwa mwanamume huyo alikaribia ua unaozunguka Ikulu katika ba… Read More

0 comments:

Post a Comment