Wednesday 24 February 2016

MCHEZAJI ALIYEMPA REFA ''KADI NYEKUNDU'' APONGEZWA…!!

Mashabiki wa kilabu Trabzonspor wamefanya maandamano, wakimuunga mkono mchezaji mmoja ambaye alipewa kadi nyekundu kwa kumuonyesha kadi nyekundi refa.

Salih Dursun alibeba kadi nyekundu na kumuonyesha refa Deniz Bitnel, na kuwa mchezaji wa nne wa Trabzonspor kutolewa nje katika mpambano aambao kilabu hiyo ilishindwa 2-1 na Galatasaray.
Hatahivyo amepata ufuasi kwa hatua yake, huku Bitnel akikosolewa kwa mchezo wake.
Trabzonspor pia imeanza kuuza fulana,zinazomuonyesha Dursun akifanya kitendo hicho.
Kumekuwa na ripoti kwamba maafisa wa kilabu hiyo huko Macka, wanapanga kujenga sanamu ya mchezaji huyo ili kuunga mkono kitendo chake.
Na huku mashabiki wa kilabu hiyo wakibeba kadi nyekundu wakiandamana huko Trabzon, mashabiki katika jimbo la magharibi la Koceli wamewasilisha malalamishi ya uhalifu kwa utumizi m'baya wa mamlaka na kuchochea chuki.
Tranzospor walikuwa chini na wachezaji tisa huku ikiwa mabao ni 1-1 wakati refa Bitnel alipompatia kadi nyekundu Luis Cavandi, kwa kucheza visivyo mbali na kuizawadi Galatasaray mkwaju wa penalti.

Wakati wa maandamano hayo dhidi ya refa uwanjani, kadi hiyo nyekundu ilianguka kabla ya Dursun kuiokota na kumuonyesha refa,ambaye alimpokonya mchezaji huyo na kumuonyesha vilevile hatua iliosababisha mchezaji huyo kuondoka uwanjani.


0 comments:

Post a Comment