Tuesday, 16 February 2016

MBUNGE ZIMBABWE AVUNJA REKODI YA BUSU AFRIKA…!!

Mbunge mmoja nchini Zimbabwe Joseph Chinotimba, ameingia katika kumbukumbu
za Afrika baada ya kumbusu mke wake Vimbai kwa muda mrefu zaidi kuwahi kurekodiwa barani Afrika.
Mbunge huyo na mkewe walizoa tuzo hiyo baada ya kupigana busu kwa dakika 10 na sekunde 17.
Rekodi hiyo iliwekwa katika hafla moja iliyopigiwa upatu na kunadiwa kuwa Mashindano ya busu refu zaidi kuwahi kutokea barani Afrika.
Hafla hiyo ilipangwa na kuandaliwa kwa ushirikiano na waandalizi wa Daftari la rekodi barani Afrika.

Hafla hiyo iliandaliwa katika mji mkuu wa Harare, kama sehemu ya kuadhimisha sikukuu ya wapendanao iliyoadhimishwa jumapili.

Related Posts:

  • VIROBA VYAPIGWA MARUFUKU ARUSHA..! Mkuu wa Mkoa wa Arusha Felix Ntibenda, amepiga marufuku uuzwaji wa kilevi aina ya kiroba katika mkoa wake. Amesema uamuzi huo unatokana na vijana ambao ni nguvu kazi ya taifa, kushindwa kufanya kazi na kulewa wakati … Read More
  • FACEBOOK YATUMIKA KUUZA SILAHA LIBYA… Utafiti mpya umebaini kwamba kuna soko linaloendelea kuimarika katika biashara haramu ya bunduki nchini Libya, kupitia mitandao ya kijamii hususan ule wa Facebook. Ripoti hiyo iliyoangazia miezi 18, ilibaini mauzo ya vi… Read More
  • LEO NI KUMBUKUMBU YA KIFO CHA AMANI ABEID KARUME… Leo April 7, 2016 ni siku ya kumbukumbu ya miaka 44 ya kifo cha Rais wa kwanza wa Zanzibar Hayati Sheikh Abeid Amani Karume ambaye alizaliwa mwaka 1905 na kufariki tarehe 7 Aprili 1972 kwa kupigwa risasi. Mzee Karume al… Read More
  • MLIMA KILIMANJARO WAIPAISHA TANZANIA KIMATAIFA.. Mlima Kilimanjaro umeendelea kuipaisha Tanzania kimataifa, baada ya kushinda kivutio cha asili Afrika kwenye Tuzo za Utalii duniani (WTA) zilizofanyika juzi visiwani Zanzibar. Mlima huo ni moja ya vipengele sita ambavyo… Read More
  • HAKIMU ‘FEKI’ ATIWA MBARONI… Mkazi wa kijiji cha Kanyama Kata ya Bujora Wilaya ya Magu mkoani Mwanza Erick Mkundi (23), ametiwa mbaroni kwa tuhuma za kufanya kazi kama Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Kongoro akiwa hana sifa hiyo. Mtuhumiwa huyo a… Read More

0 comments:

Post a Comment