Wednesday, 17 February 2016

AJABU YA MWANAMKE KUSHIKA MIMBA JELA VIETNAM..!!

Askari jela 4 nchini Vietnam wamesimamishwa kazi kwa kosa la kuzembea kazini, baada ya
mfungwa wa kike aliyehukumiwa kunyongwa kushika mimba.
Wachunguzi wanasema mfungwa huyo mwenye miaka 42, alijitungisha mimba kwa kutumia mbegu za kiume kutoka kwa mfungwa wa kiume ili kukwepa hukumu ya kifo.
Sheria ya Vietnam inasema mwanamke mjamzito au mwenye mtoto wa chini ya umri wa miaka mitatu, hawezi kunyongwa na badala yake hukumu yake inafaa kubadilishwa na kuwa kifungo cha maisha jela.
Sasa inatarajiwa kwamba hukumu yake itapunguzwa kutoka kifo hadi maisha jela, kwa sababu atakuwa na mtoto wa chini ya miaka mitatu.
Maafisa wanasema mwana mama huyo alinunua mbegu kutoka kwa mfungwa wa kiume mwenye umri wa miaka 27 kwa kati ya dollar elfu 2 na 300 na paundi elfu 1 na 600.

Mfungwa huyo alimpa mwana mama huyo mbegu zake mara mbili Agosti mwaka 2015,na mwanamke huyo anatarajiwa kujifungua mwezi Aprili.

Related Posts:

  • Mtoto apewa jina la timu ya mpira bila mama yake kujua..!! Shabiki mmoja wa Arsenal alifanikiwa kumshawishi mkewe wampe mtoto wao jina la Arsenal bila mwanamke huyo kugundua hilo. Ilikuwa ni baada ya miaka miwili ambapo mwanamke huyo Clare Smith, alijulishwa ujanja ambao mumewe … Read More
  • Homa ya Lassa yauwa 35 Nigeria.! Idadi ya watu waliopoteza maisha nchini Nigeria kutokana na ugonjwa wa homa ya Virusi vya Lassa, imeongezeka mpaka 35 kutoka watu 2 jana. Mikoa iliyoathirika na kutoa wagonjwa wengi zaidi ni pamoja na Ibadan Oyo, Taraba, … Read More
  • Choo kinachojifungua na kujiosha…! Choo cha kisasa ambacho kina uwezo wa kujifungua unapokaribia na pia kujiosha, ni moja ya vitu vinavyoonyeshwa katika maonyesho ya kimataifa ya teknolojia mpya za bidhaa za elektroniki Las Vegas. Choo hicho kilichopewa j… Read More
  • Perfume inaweza kukuletea balaa..!! Kama wewe ni kati wale ambao wanakwepa kuoga wakitegemea mtelezo wa Perfume,sikiliza hiii stori tokea huko nchini  Uingereza. Ni kwamba kijana mmoja Thomas Townsend mwenye umri wa miaka 16, amefariki d… Read More
  • Kitabu kipya cha Papa kuchapishwa…. Makao makuu ya kanisa katoliki mjini Vatican yamefichua maelezo kuhusu kitabu kipya cha papa Francis "the name of God is Mercy" jina la Mungu ni rehema, kitakachochapishwa kote duniani kwa muda wa siku mbili zijazo. Maan… Read More

0 comments:

Post a Comment