Friday 19 February 2016

TAKWIMU ZA KUNYONGWA WATU SAUDIA ZINATISHA…!!



 
Mauaji ya watu waliohukumia kifo kiholela nchini Saudi Arabia, yameongezeka katika mwaka huu wa 2016.

Gazeti la al Rayul Aam limeripoti kuwa, tangu mwanzoni mwa mwaka huu wa 2016 hadi sasa zaidi ya watu 63 wameua kwa kukatwa vichwa nchini Saudi Arabia, suala linaloakisi mwenendo wa kupanda juu takwimu za kuuliwa watu nchini humo.
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Saudi Arabia, ilitangaza jana kuwa imewanyonga watu wawili mmoja wao akiwa raia wa Yemen.
Katika mwaka uliopita Saudi Arabia iliwanyonga au kuwaua kwa kuwakata vichwa watu 153, idadi ambayo ilikuwa kubwa zaidi ya mwaka wa kabla yake kwa asilimia 80.
Saudi Arabia inakosolewa sana na jumuiya za kimataifa na taasisi za kutetea haki za binadamu, kwa kutekeleza hukumu za vifo kiholela dhidi ya wapinzani wa utawala wa kifalme wa nchi hiyo, na watetezi na wanaharakati wa kupigania haki za kijamii.

0 comments:

Post a Comment