Friday, 19 February 2016

TAKWIMU ZA KUNYONGWA WATU SAUDIA ZINATISHA…!!



 
Mauaji ya watu waliohukumia kifo kiholela nchini Saudi Arabia, yameongezeka katika mwaka huu wa 2016.

Gazeti la al Rayul Aam limeripoti kuwa, tangu mwanzoni mwa mwaka huu wa 2016 hadi sasa zaidi ya watu 63 wameua kwa kukatwa vichwa nchini Saudi Arabia, suala linaloakisi mwenendo wa kupanda juu takwimu za kuuliwa watu nchini humo.
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Saudi Arabia, ilitangaza jana kuwa imewanyonga watu wawili mmoja wao akiwa raia wa Yemen.
Katika mwaka uliopita Saudi Arabia iliwanyonga au kuwaua kwa kuwakata vichwa watu 153, idadi ambayo ilikuwa kubwa zaidi ya mwaka wa kabla yake kwa asilimia 80.
Saudi Arabia inakosolewa sana na jumuiya za kimataifa na taasisi za kutetea haki za binadamu, kwa kutekeleza hukumu za vifo kiholela dhidi ya wapinzani wa utawala wa kifalme wa nchi hiyo, na watetezi na wanaharakati wa kupigania haki za kijamii.

Related Posts:

  • Huruhusiwi kushika mimba Uchina bila ruhusa…… Kampuni moja ya Uchina inapanga kutoa masharti,ambapo wafanyikazi wake watatakiwa kupata ruhusa kabla ya kuanza familia. Sheria hizo zimechapishwa na kuzua malalamiko mengi katika mitandao. Sheria kuu inaelezea kwamba… Read More
  • Waziri aelezea hali ya ugaidi hapa nchini…… Naibu waziri wa mambo ya ndani Mheshimiwa Silima,amejibu swali juu ya hali ya ugaidi hapa nchini licha ya kifo cha kiongozi wa kundi la kigaidi Osama bin Ladden. Naibu waziri ameeleza hiyo leo bungeni mjini dodoma alipoku… Read More
  • NI VITA BUNGENI JULY 3...... Baada ya jana Bunge kuharishwa kutokana na wabunge wa upinzani kugomea nia ya kuruhusu miswada mitatu ya mafuta na gesi, kuingizwa bungeni na kujadiliwa kwa hati ya dharura, leo limehairishwa tena baada ya kubuka mz… Read More
  • Mtandao usiokubali dhambi wavutia wengi....!!! Waanzilishi wa Facegloria wanadai kwamba mtandao huo umewavutia wafuasi takriban laki moja tangu uzinduliwe mwezi Juni. Kuna maneno 600 yaliopigwa marufuku katika mtandao huo na kuna kibonyezo cha "Amen" kushabikia ujumb… Read More
  • Bunge lachafukaa.. Spika wa bunge Anna Makinda leo amelazimika kuliarisha bunge kabla ya muda wake wa kawaida, baada ya kuibuka mzozo mkali baada ya Madai ya Mbunge wa Ubungo Mhe.Mnyika, juu ya ukiukwaji wa kanuni za bunge katika kuwasilishw… Read More

0 comments:

Post a Comment