Monday 29 February 2016

WALIMU KUTOLIPA NAULI DAR ES SALAAM..

Hatimaye walimu katika jijini Dar es Salaam nchini Tanzania wataanza kusafiri bure bila ya kutozwa nauli.

Hatua hiyo ambayo itawahusu walimu wa shule za serikali, imechukuliwa katika juhudi za kutafutia ufumbuzi matatizo ya walimu kutokana na mshahara wanaolipwa kuwa mdogo na usiokidhi mahitaji.
Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Paul Makonda ameutangaza uamuzi huo wa walimu kusafiri bure wanapoelekea na kurudi kazini, baada ya ombi alilolitoa kuwaombea walimu walioko katika wilaya yake, kwa wamiliki wa mabasi hayo ya usafiri maarufu kama daladala, kukubaliwa.
Uamuzi huo utaanza kutekelezwa kuanzia Machi saba, lakini muda wao wa kusafiri bure utaanzia saa kumi na moja na nusu alfajiri hadi saa mbili alfajiri na kuanzia saa tisa hadi saa kumi na moja jioni,na kwamba zaidi ya muda huo watalipa nauli.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Madereva mkoa wa Dar es Salaam Shabani Mdemu, amesema wamekubali kuwabeba walimu bure, lakini kwa shartu wasipande wengi katika basi moja.

0 comments:

Post a Comment