Monday, 29 February 2016

WALIMU KUTOLIPA NAULI DAR ES SALAAM..

Hatimaye walimu katika jijini Dar es Salaam nchini Tanzania wataanza kusafiri bure bila ya kutozwa nauli.

Hatua hiyo ambayo itawahusu walimu wa shule za serikali, imechukuliwa katika juhudi za kutafutia ufumbuzi matatizo ya walimu kutokana na mshahara wanaolipwa kuwa mdogo na usiokidhi mahitaji.
Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Paul Makonda ameutangaza uamuzi huo wa walimu kusafiri bure wanapoelekea na kurudi kazini, baada ya ombi alilolitoa kuwaombea walimu walioko katika wilaya yake, kwa wamiliki wa mabasi hayo ya usafiri maarufu kama daladala, kukubaliwa.
Uamuzi huo utaanza kutekelezwa kuanzia Machi saba, lakini muda wao wa kusafiri bure utaanzia saa kumi na moja na nusu alfajiri hadi saa mbili alfajiri na kuanzia saa tisa hadi saa kumi na moja jioni,na kwamba zaidi ya muda huo watalipa nauli.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Madereva mkoa wa Dar es Salaam Shabani Mdemu, amesema wamekubali kuwabeba walimu bure, lakini kwa shartu wasipande wengi katika basi moja.

Related Posts:

  • Tambua madhara ya kunywa Soda Kuna mjadala mkali unaendelea kuhusu vinywaji baridi hususani soda, baada ya utafiti wa hivi karibuni kuonyesha kuwa soda inaweza kuwa na madhara zaidi kiafya kuliko hata sigara!Hii inaweza kuwa changamoto nyingine kubwa k… Read More
  • NJIA KUMI KUSAIDIA KUPUNGUZA UNENE..Kati ya sababu kuu zinazopunguza uhai wetu ni afya, unene na kutojua kujiangalia vyema.   1-ULAJI Ipo mifumo miwili ya kula. Chakula unachokula na namna unavyokila. Unavyokula. Kuna kula vyakula vidogo vidogo vyenye m… Read More
  • KWA NINI VIUMBE WENGI WANA MACHO MAWILINilikuwa natafakari juu ya uumbaji na kushangazwa na kitu kimoja cha ajabu; viumbe vingi hata vinavyoishi mazingira tofauti na vya aina (specie) tofauti sana vimefanana kwa kuwa na macho. Vinaweza vyote visiwe na miguu, mbaw… Read More
  • HIZI HAPA HASARA NA FAIDA ZA KULA NYAMA Kuna mjadala wa muda mrefu kuhusu suala la nyama nyekundu, ambapo makundi mawili tofauti yamekuwa yakitoleana hoja kuhusu faida na madhara ya kula nyama, hasa ile nyama iliyowekwa katika kundi la ‘nyama nyekundu’ (red meat)… Read More
  • JIWE LA MSINGI LA KWANZA=KIWA                 KIWA STRONG- Knowledge Inteligent With Action=KIWA Katika maisha siku zote ni kutokukata tamaa katika jambo unalolifanya,hiyo ndiyo siri ya mafanikio sababu yoyot… Read More

0 comments:

Post a Comment