Wednesday, 10 February 2016

UTAFITI: FARASI HUBAINI HISIA ZA MWANADAMU..!

Farasi huweza kubaini kati ya mtu aliye na furaha na aliye kasirika, kwa kuangalia uso wa mwanadumu utafiti umesema.

Katika jaribio kwa kutumia picha za mwanamume wanasayansi kutoka chuo kikuu cha Sussex, walionyesha kwamba farasi wanaofugwa nyumbani huchukizwa na sura zilizokasirika.
Wanasayansi hao wanasema kuwa ufugaji huo, huenda umewawezesha farasi kuelewa tabia za binaadamu.
Matokeo hayo yamechapishwa katika jarida la Biology Letters.
Kundi hilo lilifanya vipimo vyake kwa kuwasilisha picha nyingi mbele ya farasi 28.
Matokeo yake alielezea ni kwamba waliangalia picha za watu waliokasirika na jicho lao la kushoto.
Akili za wanyama zimeumbwa kana kwamba hisia zinazotolewa na jicho la kushoto, huangaziwa na eneo la kulia la ubongo ambalo hutumiwa kuangazia hisia mbaya.
Watafiti hao pia waliweka vipimo vya moyo katika moyo wa farasi hao, ambavyo vilibaini kwamba nyuso zilizokasirika hufanya moyo wa wanyama husika kudunda kwa haraka.

Matokeo kama hayo yameripotiwa miongoni mwa mbwa, na kuzua maswali kuhusu ni vipi kuishi na binaadamu kuna badili tabia za wanyama hao.

Related Posts:

  • Pakua ngoma mpya ya Same Girls hapa.!! Nimekuwekea hapa wimbo mpya wa Same Girls unakwenda kwa jina la More baby unaweza kuusikiliza ama kuupakua hapa chini onyesha saport yako kwa vijana hawa. … Read More
  • Hizi ndizo story zilizoko kwenye Headlines leo May 11 TZ: JWTZ wanasubiri kupokea miili ya wanajeshi waliofariki DRC Congo, Waziri Mkuu Pinda atakabidhiwa ripoti ya maafa ya mvua Dar leo, Kafulila ameapa kuibua ishu ya ESCROW upya, anaituhumu Ikulu kuwasafisha watuhumiwa. … Read More
  • Kwa bei ya sh.500/= utayajua magonjwa sugu 8 ambayo yanatibiwa kwa mbegu za tikiti maji, usikose nakala yako ya gazeti la Tabibu wiki hii.  Katika michezo fahamu maisha ya Simon Msuva na mengine mengi. … Read More
  • Wanasayansi watengeza mbegu za kiume!!!!!! Seli za mbegu za kiume zimetengezwa katika maabara kwa mara ya kwanza na hivyo basi kuwapa matumaini wanaume wasio na uwezo wa kupata watoto. Kampuni moja nchini Ufaransa imedai kwamba imefanikiwa kubadilisha vipande t… Read More
  • Kanisa labadilishwa kuwa msikiti Itali..!!!! Iceland imezua hisia kali wakati wa ufunguzi wa maonyesho ya usanii katika mji wa Venice nchini Italy baada ya kulibadilisha kanisa ambalo lilikuwa halitumiki kuwa msikiti. Kwa jina 'La Moschea' msikiti huo… Read More

0 comments:

Post a Comment