Monday, 22 February 2016

MAREKANI YAONGOZA KWA BIASHARA YA SILAHA…!

Usafirishaji wa silaha duniani umeongezeka katika miaka ya hivi karibuni, huku Marekani ikiendelea
kuongoza katika biashara ya silaha na Urusi ikiwa ya pili.
Kwa mujibu wa ripoti ya utafiti mpya wa taasisi ya kimataifa ya amani mjini Stockholm nchini Sweden SIPRI, silaha zilizosafirishwa barani Afrika, Asia na Mashariki ya Kati zimeongezeka.
Ripoti hiyo inasema kiwango cha silaha kubwa zilizosafirishwa, kilikuwa asilimia 14 zaidi katika kipindi cha kati ya mwaka 2011 na 2015, ikilinganishwa na miaka mitano kabla, huku Marekani na Urusi zikisafirisha silaha nyingi.
Nchi zilizoagiza silaha nyingi ni India, Saudi Arabia, China na Falme za Kiarabu.

Watayarishaji wa ripoti hiyo waliuzungumzia mzozo wa Yemen wakisema muungano wa nchi za kiarabu unaopambana na waasi wa Houthi nchini humo, unatumia silaha nzito za kisasa kutoka Marekani na Ulaya. 

Related Posts:

  • BIBI YAKE OBAMA AENDELEA KUPEWA ULINZI..! Bibi yake na Rais wa Mstaafu wa Marekani, Barack Obama, Bi, Saraha Obama ataendelea kupewa ulinzi licha ya mjukuu wake kumaliza muhula wa uongozi wake wiki iliyopita. Kwa mujibu wa gazeti la The Standard, limewak… Read More
  • KUSOMA KWA NJIA YA MTANDAO KWAZIDI KUSHIKA KASI... DUNIA inakimbia kwa kasi ya ajabu mno! Hii inadhihirishwa na mabadiliko mbaliambali ya mifumo ya maisha ya kila siku. Kadri siku zinavyozidi kwenda, ndivyo utandawazi unazidi kujitangazia ushindi, kwani mambo mengi yanah… Read More
  • MLANGO WA BOMBARDIER WAZUA TAHARUKI ANGANI…! Abiria waliokuwa wakisafiri kwa ndege aina ya Bombardier Q400 ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) kutoka Mwanza kuelekea Dar es salaam, walipata hofu baada ya ndege yao kuruka na muda mfupi baadae kulazimika kutua tena ka… Read More
  • CHAGUO LA MAKAMU WA URAIS LAZUA UTATA GAMBIA...! Rais mpya wa Gambia Adama Barrow amemteua mwanamke mwenye ushawishi mkubwa, ambaye aliwahi kuwa mshirika wa aliyekuwa rais wa taifa hilo Yahya Jammeh kabla ya kujiunga na upinzani ulioshinda uchaguzi kuwa makamu wake wa… Read More
  • NYAMA KUANZA KUTENGENEZWA MAABARA.. DUNIA inabadilika kwa haraka kutokana na maendeleo katika sekta mbalimbali. Teknalojia nayo inakua kwa kasi huku ikitoa mchango mkubwa katika maendeleo ya binadamu. Siku hizi Dunia inashuhudia uvumbuzi wa teknalojia za ki… Read More

0 comments:

Post a Comment