Monday 22 February 2016

MAREKANI YAONGOZA KWA BIASHARA YA SILAHA…!

Usafirishaji wa silaha duniani umeongezeka katika miaka ya hivi karibuni, huku Marekani ikiendelea
kuongoza katika biashara ya silaha na Urusi ikiwa ya pili.
Kwa mujibu wa ripoti ya utafiti mpya wa taasisi ya kimataifa ya amani mjini Stockholm nchini Sweden SIPRI, silaha zilizosafirishwa barani Afrika, Asia na Mashariki ya Kati zimeongezeka.
Ripoti hiyo inasema kiwango cha silaha kubwa zilizosafirishwa, kilikuwa asilimia 14 zaidi katika kipindi cha kati ya mwaka 2011 na 2015, ikilinganishwa na miaka mitano kabla, huku Marekani na Urusi zikisafirisha silaha nyingi.
Nchi zilizoagiza silaha nyingi ni India, Saudi Arabia, China na Falme za Kiarabu.

Watayarishaji wa ripoti hiyo waliuzungumzia mzozo wa Yemen wakisema muungano wa nchi za kiarabu unaopambana na waasi wa Houthi nchini humo, unatumia silaha nzito za kisasa kutoka Marekani na Ulaya. 

0 comments:

Post a Comment