Friday 5 February 2016

MGODI WAPOROMOKA AFRIKA KUSINI…

Takriban wachimba mgodi 52 wamekwama ardhini, ndani ya mgodi wa dhahabu mashariki mwa Afrika Kusini kulingana na chombo cha habari cha News24.

Kisa hicho kilitokea mwendo wa saa mbili asubuhi,kulingana na daktari mmoja wa kutoa matibabu ya dharura Jacques Ainslie.
Mojawapo ya shimo liliporomoka na kuwanasa wachimba mgodi 52.
Kufikia sasa asilimia 70 ya wachimba mgodi hao ama wafanyikazi 30 wameokolewa,bwana Ainslie alikiambia chombo cha habari cha News24.
Wachimba mgodi waliojeruhiwa wamesafirishwa katika hospitali moja kwa matibabu.
Hatahivyo watu watatu bado hawajulikani waliko, na bwana Anslie amesema anashuku huenda wamekwama katika chumba ambapo mporomoko huo ulianza.


0 comments:

Post a Comment