This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Thursday 22 March 2018

SERIKALI YAMWONYA DIAMOND……

 

Wizara ya Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo nchini Tanzania imemshutumu nwanamuziki maarufu Diamond Platnumz kwa kauli aliyoitoa kuhusu kufungiwa kwa nyimbo zake mbili.

AMUUA MAMA YAKE KISHA KUMTOA MACHO….

Camille Balla 32, kutoka Florida amekamatwa baada ya kumuua mama yake Francisca Monterio-Balla na kisha kumtoa macho na kisha kupiga simu polisi na kuwaeleza kuwa yeye ni muuaji.

WAZIRI ASIMAMISHWA KAZI KWA KUMPIGA MBUNGE…

Bunge la Zambia limemsimamisha kazi Waziri wa Jimbo la Lusaka Bowman Lusambo kwa muda wa mwezi mmoja, baada ya kumchapa kibao mbunge Chishimba Kambwili wakiwa bungeni.

MSICHANA ALIYEWAPIGA MAKOFI WANAJESHI AFUNGWA JELA…

Msichana wa Palestina Ahed Tamimi aliyerekodiwa kwenye kipande cha video akizozana na baadaye kuwapiga makofi wanajeshi wa Israel wenye bunduki, amehukumiwa kifungo cha miezi nane jela baada ya kukiri makosa.

WABUNGE WAFYATUA GESI YA MACHOZI BUNGENI....

Wabunge wa kambi ya upinzani katika Bunge la Kosovo wamefyatua gesi ya machozi bungeni wakati vikao vya bunge vikiendelea, kwa lengo la kuzuia bunge hilo kupitisha mkataba wasioupenda.

Friday 16 March 2018

RAIA WA TANZANIA NA BURUNDI HAWANA FURAHA….

Tanzania, Burundi na Rwanda zimeorodheshwa kuwa kati ya nchi zenye watu wasio na furaha duniani katika orodha ya kila mwaka ya Umoja wa Mataifa kuhusu viwango vya furaha duniani.

MUGABE: SIKUTEGEMEA KUONDOLEWA MADARAKANI NA MNANGAGWA

 

Aliyekua Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe, amevunja ukimya kwa mara ya kwanza tangu aondolewe Madarakani,kwa kusema kuwa amekua muhanga wa mapinduzi ya kijeshi.

Monday 12 March 2018

MAMA AJINYONGA BAADA YA KUUA WANAWE WANE……

Mwanamke mmoja katika kijiji cha Nyahera Kaunti ya Kisumu nchini Kenya, amewaua watoto watatu wa mke mwenzie, na kisha mwenyewe kujinyonga.

NKURUNZINZA ATANGAZWA KUWA KIONGOZI WA MAISHA…..

Chama tawala nchini Burundi CNDD/FDD kimemtangaza Rais Pierre Nkurunzinza, kama kiongozi mkuu wa kudumu au kiongozi wa milele ndani ya chama hicho.

Wednesday 7 March 2018

KAMANDA WA POLISI AKANUSHA KUPATIKANA KWA MASHEIKH ZANZIBAR..


Jeshi la Polisi Zanzibar limesema halina taarifa za kuonekana kwa mashekhe watatu wa Jumuiya ya Maimamu Zanzibar, ambao waliripotiwa kutoonekana tangu Januari 9, mwaka huu.

UNAFAHAMU UMRI SAHIHI WA KUANZA KUFANYA MAPENZI NCHINI MWAKO..?

Ufaransa inatarajia kuweka sheria maalum ya umri wa kuanza kufanya mapenzi kuwa ni miaka 15.

Hivyo kufuatia mapendekezo hayo mtu yeyote atakayebainika kufanya mapenzi chini ya umri huo atakuwa amebaka.

Maamuzi haya yamekuja nchini humo mara baada ya madaktari na wanasheria kutoa ushauri wao kuhusiana na umri mtu anaostahili kuanza kufanya mapenzi.

MHUBIRI AWAVUTIA WAUMINI KWA KUTEMBEA HEWANI....

Mhubiri mmoja nchini Malawi amewavutia  waumini wake kwa kudaiwa kuwa anatembea hewani, kuponya walioathirika na ukimwi, kuponya vipofu na kuwaombea masikini kuwa matajiri.

Tuesday 6 March 2018

WAANDAMANA KUOMBA RAIS ADHIBITI ULEVI WA WANAUME….

Mamia ya wanawake katika vijiji vya Kirangi na Kuri Kiambu nchini Kenya, wameandamana Jumapili iliyopita wakipinga ongezeko la vilabu vya pombe (bars) na ulevi wa waume zao.

WACHUNGAJI 6 WA MAKANISA YALIYOFUNGWA RWANDA WAKAMATWA..

Polisi nchini Rwanda imetangaza kuwatia kizuizini wachungaji 6 na viongozi wa makanisa, kutoka baadhi ya makanisa yaliyofungwa kwa amri ya serikali ya nchi hiyo.

AOMBA KUPELEKWA KWA MGANGA BADALA YA JELA…….

Mwanaume mmoja kwa jina la Wilson Obeka anaekabiliwa na mashtaka ya jinai, aliwashangaza wengi mahakamani huko Eldoret baada ya kumuomba hakimu apelekwe kumuona mchungaji au mganga badala ya kwenda jela.

VIDEO: MOTO WATEKETEZA SOKO LA MBAGALA….

Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu–Dar, asubuhi ya leo Machi 6, 2018.

Monday 5 March 2018

INSPEKTA WA POLISI NA WAZIRI WA ULINZI WAFUKUZWA KAZI…

Rais wa Uganda Yoweri Museveni, amemfuta kazi Inspekta mkuu wa polisi Kale Kayihura na waziri wa Ulinzi Henry Tumukunde.

Sunday 4 March 2018

WATU WAPIGA KURA UCHAGUZI MKUU ITALIA…

Watu nchini Italia wanapiga kura baada ya kampeni zilizoangazia zaidi masuala la uhamiaji na uchumi.

TMA YATOA TAHADHARI KWA WANANCHI…….

Mamlaka ya hali ya hewa iliyopo chini ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano nchini Tanzania imewatahadharisha wananchi kuwepo kwa hali mbaya ya hewa katika maeneo yote ya pwani kuanzia leo usiku.

MWANAFUNZI MTANZANIA AUAWA KIKATILI AFRIKA KUSINI………….

Mwanafunzi wa Tanzania aliyekuwa akisoma nchini Afrika Kusini,Baraka Nafari aliyekuwa akichukua Shahada ya Uzamivu (PHD) katika Chuo Kikuu cha Johannesburg (UJ) ameuawa kikatili Ijumaa Februari 23, mwaka huu kwa kugongwa na gari mara mbili na kubamizwa kwenye ukuta na baadaye kushambuliwa kwa visu.

MWANAMUME AJIPIGA RISASI NA KUJIUA NJE YA WHITE HOUSE….

Mwanamume mmoja amejipiga risasi na kujiua nje ya Ikulu ya Marekani ya White House mjini Washington, kikosi cha kumlinda rais kimesema.