Friday 16 March 2018

RAIA WA TANZANIA NA BURUNDI HAWANA FURAHA….

Tanzania, Burundi na Rwanda zimeorodheshwa kuwa kati ya nchi zenye watu wasio na furaha duniani katika orodha ya kila mwaka ya Umoja wa Mataifa kuhusu viwango vya furaha duniani.Burundi ndilo taifa ambalo wakazi wake hawana furaha zaidi duniani katika nafasi ya 156 ambapo imechukua nafasi hiyo kutoka kwa Jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR) iliyokuwa inashikilia nafasi hiyo mwaka jana.CAR ndiyo inayoifuata Burundi katika orodha ya mwaka huu.Tanzania imeshika nafasi ya 153 sawa na mwaka jana huku Rwanda pia ikishikilia nafasi ya 151 sawa na mwaka jana kati ya mataifa 156.Orodha ya mwaka jana hata hivyo ilishirikisha mataifa 155.Taifa linaloongoza kwa furaha duniani mwaka huu ni Finland, kwa mujibu wa ripoti hiyo ya UN ambapo nchi hiyo imechukua nafasi hiyo kutoka kwa Norway.Ripoti hiyo huangazia furaha waliyo nayo watu wa taifa furahi na chanzo cha furaha hiyo.Mataifa ya Ulaya Kaskazini yanashikilia nafasi tano za juu kwa kuwa na viwango vya juu vya raia walioridhika, huku nchi zilizoathiriwa na vita vya muda mrefu pamoja na nchi kadha za Afrika Kusini mwa Sahara zikiendelea kwa mara nyingine kushikilia nafasi tano za chini.

0 comments:

Post a Comment