Monday 12 March 2018

NKURUNZINZA ATANGAZWA KUWA KIONGOZI WA MAISHA…..

Chama tawala nchini Burundi CNDD/FDD kimemtangaza Rais Pierre Nkurunzinza, kama kiongozi mkuu wa kudumu au kiongozi wa milele ndani ya chama hicho.

Uamzi huo umefikiwa baada ya vikao vya siku tatu vya mkutano mkuu wa chama hicho uliofanyika katika eneo la Buye anakozaliwa Bwana Nkurunziza Kaskazini mwa nchi hiyo.
Uamuzi huo pia unachukuliwa wakati Burundi inajiandaa kufanya marekebisho ya katiba, ili kumruhusu Rais Nkurunzinza kuendelelea kuongoza taifa hilo hadi mwaka 2034.
Taaarifa ya chama cha CNDD/FDD imesema kuwa, vikao hivyo vilinuwia kuimarisha chama tawala na taasisi zake.

0 comments:

Post a Comment