Rais wa Uganda Yoweri Museveni, amemfuta kazi
Inspekta mkuu wa polisi Kale Kayihura na waziri wa Ulinzi Henry Tumukunde.
Generali Kayihura
ambaye ni mkereketwa wa vita vilivyomsaidia rais Museveni kuingia madarakani
mwaka 1986, kwa wakati mmoja alikisiwa kuwa afisa mwenye mamlaka makubwa zaidi
katika jeshi la Uganda.
Lakini
amekabiliwa na shinikizo kwa kushindwa kukabiliana na ukosefu wa usalama.
Zaidi ya wanawake 20
wameuawa katika visa vya mauaji, ambavyo havijatatuliwa katika maeneo
yanayouzunguka mji mkuu wa Kampala, na katika miezi mitatu iliyopita raia
watatu wa kigeni pia wameuawa.
Naibu
wake Okoth Ochola anashikilia wadhifa huo.
Kwa mujibu wa ujumbe
alioandika rais Museveni katika mtandao wa Twitter, amesema: "Kwa uwezo wa
mamlaka niliyopewa kikatiba, nimemteua Jenerali Elly Tumwiine kama waziri wa
usalama.Nimemteua pia bwana Okoth Ochola kama afisa mkuu wa polisi. Niabu wake
atakuwa ni Brigedia Sabiiti Muzeei.
Mnamo Mei mwaka 2017
Rais Museveni alimteua upya Kayihura kama mkuu wa polisi kwa muhula mwingine wa
miaka mitatu hadi mwaka 2020.
Uteuzi huo ulikumbwa
na mzozo na haukudumu.
0 comments:
Post a Comment