Moto
mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga)
katika eneo la Mbagala Rangi Tatu–Dar, asubuhi ya leo Machi 6, 2018.
Sehemu
iliyoathirika zaidi ni ya wauza mitumba huku baadhi ya bidhaa zao zikiteketea
kwa moto lakini hakuna aliyeripotiwa kupoteza maisha wala kujeruhiwa.
Chanzo
cha moto huo kinadhaniwa kuwa ni hitilafu ya umeme ambapo tayari gari la jeshi
la zima moto limefika kuzima moto huo.
0 comments:
Post a Comment