Polisi nchini Rwanda imetangaza kuwatia kizuizini
wachungaji 6 na viongozi wa makanisa, kutoka baadhi ya makanisa yaliyofungwa
kwa amri ya serikali ya nchi hiyo.
Wiki iliyopita serikali ya nchi hiyo iliamrisha
kufungwa kwa makanisa zaidi ya 700, kwa madai ya kutotimiza kanuni za ujenzi wa
makanisa yao.
Miongoni mwa waliokamatwa ni kasisi Askofu Innocent
Rugagi, kiongozi wa kanisa la Abacunguwe ambaye ni mojawapo ya wachungaji
mashuhuri nchini Rwanda.
Polisi inawashutumu kwa kufanya mikutano ya siri
kukaidi uamuzi wa serikali.
0 comments:
Post a Comment