Mwanamume mmoja amejipiga risasi
na kujiua nje ya Ikulu ya Marekani ya White House mjini Washington, kikosi cha
kumlinda rais kimesema.
Kikosi hicho kilisema kuwa mwanamume
huyo alikaribia ua unaozunguka Ikulu katika barabara ya Pennsylvania kabla ya
kuchomoa bunduki na kupiga risasi mara kadhaa.
Hakuna mtu aliyejeruhiwa, kulingana
na polisi.
Rais Donald Trump hakuwa kwenye
Ikulu. Yuko katika kasri lake la Mar-a-Lago huko Florida.
Mwanamume huyo alikuwa kwenye watu
wengi wakati alipiga risasi, kulingana na wale walioshuhudia,na jina lake bado
halijatangazwa.
Video iliyochapishwa kwenye mtandao
wa Twitter ilionyesha watu wengi wakikimbia kutoka eneo hilo.
Kumekuwa na visa kadha vinavyohusu
usalama katika Ikulu ya White House miaka ya hivi karibuni.
Cha hivi karibuni tarehe 23
Februari, gari liliendeshwa kwenda kwa kizuizi cha Ikulu ambapo mwanamke wa
miaka 35 alikamatwa.
0 comments:
Post a Comment