Camille Balla 32, kutoka
Florida amekamatwa baada ya kumuua mama yake Francisca Monterio-Balla na kisha
kumtoa macho na kisha kupiga simu polisi na kuwaeleza kuwa yeye ni muuaji.
Hii ilitokea baada ya binti
huyo kutumia madawa ya kulevya yaliompelekea kutokujielewa.
Baada ya polisi kufika eneo
la tukio walikuta mwanamke huyo amekaa huku damu zikiwa zimetapakaa.Aliamka na
kukimbia ndani ya nyumba na kisha kudai kuwa
yeye ni muuaji.⠀
Mwanamke huyo alikamatwa na
kudai kuwa alikuwa amevuta bangi kabla ya kumvamia mama yake na kisha kumuua.Jumatatu
alikutanishwa na hakimu jumatatu lakini alinyimwa dhamana kutokana na kile
alichokifanya.
0 comments:
Post a Comment