Home »
Kimataifa
» MUGABE: SIKUTEGEMEA KUONDOLEWA MADARAKANI NA MNANGAGWA
Aliyekua Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe, amevunja
ukimya kwa mara ya kwanza tangu aondolewe Madarakani,kwa kusema kuwa amekua
muhanga wa mapinduzi ya kijeshi.Akiongea na televisheni ya SABC ya Afrika kusini,
Mugabe amesema Rais wa sasa Emerson Mnangagwa asingeweza kuingia madarakani
bila kutumika kwa jeshi.Akiwa katika nyumba yake ya kifahari mjini Harare,
Mugabe amekemea mbinu zilizotumika kumuondoa madarakani..Amesema alikua tayari kufanya mazungumzo na Rais wa
sasa Emerson mnangagwa na angehakikisha mabadiliko ya madaraka ya uhalali na si
yale ya kulazimishwa.Mugabe amesema kuwa Yuko tayari kwa ajili ya
Mazugumzo na Mnangagwa ili kulinda katiba yao.Hakuna uhakika kama rais huyo wa zamani mwenye Umri
wa miaka 94 Anataka kurudi madarakani ama la, lakini ni wazi kuwa anadhani
amesalitiwa na rais wa sasa Emerson Mnangagwa.
0 comments:
Post a Comment