Thursday 22 March 2018

SERIKALI YAMWONYA DIAMOND……

 

Wizara ya Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo nchini Tanzania imemshutumu nwanamuziki maarufu Diamond Platnumz kwa kauli aliyoitoa kuhusu kufungiwa kwa nyimbo zake mbili.

Waziri Dkt Harrison Mwakyembe amesema "amesikitishwa" na kauli alizozitoa mwanamuziki huyo akihojiwa na kituo kimoja cha redio jijini Dar es Salaam.
Waziri huyo amesema maamuzi ya kuzifingia baadhi ya nyimbo na wasanii wawili kwa kukiuka maadili yalifanywa kwa mujibu wa sheria na siyo kwa utashi wa Naibu Waziri Juliana Shonza.
Mwanamuziki huyo wa kizazi kipya, ambaye jina lake halisi ni Nassib Abdul, anadaiwa kumlaumu naibu huyo wa waziri.
"Diamond atambue kuwa serikali ina taratibu zake na maamuzi ya naibu waziri ni maamuzi ya wizara," Dkt Mwakyembe amenukuliwa kwenye taarifa iliyotumwa na wizara hiyo kwa vyombo vya habari.
Nyimbo za Diamond zilizofungiwa na Mamlaka ya Mawasiliano nchini Tanzania (TCRA) mwishoni mwa mwezi uliopita ni Hallelujah (uliomshirikisha Morgan Heritage ) na Waka Waka (uliomshirikisha Rick Ross).
Waziri huyo alisema kuna vikao vingi vya wasanii ambavyo vimekuwa vikifanywa kati ya serikali na wasanii "lakini Diamond hakuwahi kuhudhuria vikao hivyo."
"Si wajibu wa serikali kumfanyia kikao cha peke yake."
"Sheria ni ya watu wote bila kujali umaarufu au nafasi ya mtu katika jamii, hivyo msanii Diamond anapaswa kutii sheria na mamlaka zilizowekwa."
Waziri huyo alimwambia mwanamuziki huyo kwamba si busara kwake kushindana na serikali na kwamba endapo ana ushauri wowote, ni vyema kwake kuuwasilisha kwa njia sahihi "lakini si kwa kumshambulia waziri kwa dharau na kejeli kama alivyofanya."
Dkt Mwakyembe alisema Diamond anatarajiwa kuwa mfano bora kwa wanamuziki wenzake kutokana na mafanikio aliyoyapatta katika fani ya muziki.
"Napenda kuwakumbusha wasanii wote kwamba sanaa ni kazi kama zilivyo kazi nyingine, hivyo pamoja na kuwa na kipaji hicho, wasanii wanatakiwa kuzingatia sheria, kanuni na miongozo inayosimamia tasnia ya sanaa kama ilivyo kwa tasnia nyingine," alisema Dkt Mwakyembe.
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) na Chama cha Wasanii wa Muziki wa Bongo Fleva (Tuma) na Waziri wa Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo, pia walishutumu hatua ya mwanamuziki huyo ya kumshambulia naibu waziri huyo.

TCRA nayo ilisema kuwa inafuatilia mahojiano yake katika kituo hicho kazi ambayo inafanywa na kamati yake ya maudhui, kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi.
Afisa Mkuu Idara ya Utangazaji TCRA, Andrew Kisaka alisema wamechukua uamuzi huo kwa kuwa mahojiano hayo yamefanyika katika kituo wanachokisimamia.
Kwa mujibu wa gazeti hilo la Mwananchi, Bw Kisaka alisema mamlaka hiyo inanaangalia zaidi chombo ambacho imekipa leseni na kwamba, masuala mengine yatashughulikiwa na mamlaka nyingine.
Basata kupitia katibu mtendaji wake, Godfrey Mngereza walimtaka Diamond kufuata taratibu katika kulalamikia suala hilo ikiwamo kuandika barua kama alivyoelezwa.
Alisema si lazima msanii aandikiwe barua pale anapokosea kama ambavyo Diamond alitaka kupitia ukurasa wake wa Twitter katika ujumbe aliouandika Jumanne.
Diamond aliandika: "Swala la Barua Unalijua leo baada ya Kukosa Point sahihi?
Ungekuwa unajua kama taratibu sahihi ni Kuandika Barua, Mbona hukuwatumia pia Wasanii barua zakuwa unafungia kazi zao?... kwakuwa Uliyapeleka Social Media na Radio, nami nikakupelekea huko ili uenjoy Zaidi...


0 comments:

Post a Comment