Mamia ya wanawake katika vijiji vya Kirangi na Kuri Kiambu nchini
Kenya, wameandamana Jumapili iliyopita wakipinga ongezeko la vilabu vya pombe
(bars) na ulevi wa waume zao.
Wakizungumza wakati wa maandamano hayo ya amani, wanawake zaidi ya 100 wa
eneo hilo, walionesha hasira zao dhidi ya ulevi wa wanaume na watoto wao wa
kiume.
Ombi la wanawake hao kwa Rais Uhuru Kenyatta, ni kuwachukulia hatua
maafisa wa jeshi la polisi katika eneo hilo, ambao wanadaiwa kupokea rushwa ili
kulinda kumbi za starehe na bar katika eneo hilo tofauti na jitihada za
Serikali kudhibiti ulevi hasa wa pombe haramu.
Walidai wanaume wao wamekuwa dhaifu wanaoshindwa kutimiza wajibu wao wa
kifamilia, wengi wao wamekimbia nyumba zao.
Waliongeza kuwa wengine walifikia hatua ya kuuza mali zao ili wapate
pesa ya kununua pombe.
Maandamano hayo yamekuja wakati ambapo Serikali ya Kenya imeanza
oparesheni ya kuharibu vifaa vya kutengeneza pombe haramu na kuwakamata
wahusika.
0 comments:
Post a Comment