Friday 24 July 2015

Korea kaskazini yatoa utaratibu mpya kila ikifika saa 11 Alfajiri……

 
Kama ulikuwa hufahamu ni kwamba Korea Kaskazini sasa hivi hali ya hewa ni joto sana, lakini yapo mengine toka huko ambapo msimu huu wa joto kali umepewa jina la Sambok.

Limetolewa agizo na serikali kuwa, Ofisi zote, shule na kila taasisi nchi nzima, zinatakiwa kufuata ratiba mpya ambayo Serikali imeweka.

Ratiba hiyo mpya ya sasa ni kwamba kila kitu kitaanza kufanya kazi saa 11 asubuhi badala ya saa mbili asubuhi, na mwisho wa shughuli zote ni saa saba mchana, hilo ni agizo jipya la Serikali ya Korea Kaskazini.

Wastani wa joto la Korea ni kama 29˚ Centrigrade lakini kwa sasa imefikia mpaka 40˚ Centigrade.

Hii sio mara ya kwanza kutangazwa utaratibu huo, kwani wakati Rais Kim Jong-il akiwa madarakani uliwahi kutangazwa utaratibu wa aina hii pia.

Htari nyingine ni kwamba Maofisini kwenye AC na feni, huenda hii isiwe taarifa nzuri kwao, huku joto likiwa limekuwa kali na hakuna maji ya kutosha kwenye vyanzo vya umeme sasahivi, kwa hiyo ishu ya feni na AC kufanya kazi ofisini huenda ikawa kitendawili.

Watu wengi hawajapenda hiyo ratiba mpya, unaambiwa mpaka Migahawa ya Serikali inatoa huduma mwisho mchana, ukienda jioni au usiku hakuna huduma utakayopata!!

0 comments:

Post a Comment