Wednesday 15 July 2015

NASA wapata taarifa za Sayari ya Pluto……

Wana sayansi wa NASA kutoka Marekani wanasema kuwa,majaribio yao ya kurusha chombo kwenda katika sayari ya Pluto yamekuwa na mafanikio makubwa.

Chombo hicho kimefanikiwa kutuma taarifa katika kituo cha utafiti huo cha Maryland, zilizochukua takribani saa nne na nusu hadi kufika duniani na kupokelewa na antenna NASA.

Saa chache zijazo wanasayansi hawa wa NASA wameeleza kuwa, wanatarajia kupata mfululizo wa taariza zaidi na picha kutoka sayari hiyo ya Pluto ambazo zitatoa uhalisia wa undani wa sayari hiyo ya Pluto.

0 comments:

Post a Comment