Friday 24 July 2015

Sayari nyingine yagunduliwa…

Wanasayansi wa taasisi ya Marekani ya Uchunguzi wa Anga NASA, wamegundua sayari inayofanana kwa karibu zaidi na dunia kuliko sayari nyingine zote.

Sayari hiyo iliyopewa jina la Kepler 452-b ina umri wa miaka bilioni 6, na inazunguka nyota inayofanana na jua linalozungukwa na dunia.
Wanasayansi wa NASA wanaamini kwamba upo uwezekano wa viumbe hai, kuishi katika sayari hiyo.
Kepler 452-b imegunduliwa na chombo cha upelelezi wa anga kinachoitwa Kepler.

Chombo hicho kilirushwa angani mwaka 2009 kwa lengo la kutafuta sayari zenye vigezo vinavyofanana na dunia.

0 comments:

Post a Comment