Thursday 16 July 2015

Picha ya kwanza kutoka sayari ya Pluto……

Picha ya kwanza inaonyesha kwa undani sayari ya Pluto ilivyo imeonyeshwa kwa mara ya kwanza duniani.

Picha hiyo imepigwa na chombo kisicho na binadamu kilichotumwa kwenye safari hiyo ambacho kilisafiri umbali wa kilometa bilion saba na tano.
Chombo hicho jana jumanne kilitua kwenye sayari hiyo.
Katika mkutano na waandishi wa habari katika chuo Kikuu cha Johns Hopkins kilichopo Maryland Marekani, Mkuu wa utafiti wa sayari hiyo Alan Stern hakusita kuonyesha furaha yake.
"Jana ilikuwa ni siku nzuri na ya kipee kwangu, vipi kwenu."
Mkuu huyo wa utafiti Alan Stern amesema chombo hicho cha anga kimekusanya taarifa nyingi kutoka kwenye sayari hiyo.
"Sawa chombo chetu cha New Horizons kimekwenda sasa zaidi ya mile milioni moja.
Zaidi ya kilometa moja na nusu upande wa pili wa Pluto, hivyo ndivyo tunavyokwenda kwa haraka tumefikia karibu na sayari hiyo hapo jana asubuhi.
Chombo chetu cha anga kipo katika hali nzuri, kinafanya mawasiliano na dunia kwa mara nyingine mara kwa mara kwa masaa kuanzia asubuhi saa 11 na dakika 50.

Tayari tumepata data kutoka kwenye vifaa vya kisayansi vipatavyo vitano, na tutatoa taarifa kuhusu matokeo tuliyopata, lakini ukweli ni kwamba tunachunguza kwa undani, kuna mengi." Amesema Alan Stern.

0 comments:

Post a Comment