Wednesday 8 July 2015

Mwanamme mzee zaidi duniani aaga dunia…!!!

Mwanamme mzee zaidi duniani raia wa Japan Sakari Momoi, ameaga dunia mjini Tokyo akiwa na umri wa miaka 112.

Mwalimu huyo mkuu wa zamani wa shule ya upili na baba wa watoto watano, aliaga dunia kutoka na ugonjwa wa figo katika kituo kimoja cha kuwahudumia watu wazee siku ya Jumapili.
Alikuwa ametambuliwa na Guinness World Records mwezi Agosti.
Momoi alizaliwa mwaka 1903 mjini Fukushima na alikuwa mwalimu kabla ya kupanda cheo na kuwa mwalimu mkuu kwenye shule kadha nyumbani kwao.
Wakati alipopata cheti kutoka kwa Guinness World Records mwezi Agosti, aliwaambia waandishi wa habari alitaka kuishi miaka miwili zaidi.
Guinness bado haijatangaza mwanamamme mwenye umri mkubwa zaidi duniani baada ya Momoi.

Mtu ambaye aliishi miaka mingi zaidi duniani kulingana na Guinness ni Jeanne Calment kutoka ufaransa ambaye aliishi miaka 122 na siku 164.Aliaga dunia mwezi Agosti mwaka 1997.

0 comments:

Post a Comment