Wednesday 15 July 2015

Wabunge wa Rwanda wamuunga mkono Kagame kugombea muhula wa tatu..

Wabunge wa Rwanda wamepiga kura jana Jumanne kuunga mkono mabadiliko ya katiba, ili kumruhusu rais Paul Kagame awanie muhula wa tatu madarakani, wakiunga mkono waraka ulotiwa saini na mamilioni ya raia.

Bunge zima lililojaa wananchi waliokwenda kushuhudia utaratibu mzima, lilisherehekea na kuimba jina la Kagame baada ya wabunge wote waliokuwepo katika mabaraza yote mawili ya bunge kupiga kura katika hatua ya kwanza ya utaratibu kwa ajili ya mabadiliko ya katiba.
Spika wa bunge Donatillla Mukabalisa, amesema kwa maneno yake “ninataka kuwashukuru wabunge wote kwa kuonyesha uungaji mkono matarajio ya wananchi”.

Zaidi ya watu milioni 3.7 ambao ni zaidi ya nusu ya wapiga kura walitia saini nakala ya kutoa wito kwa mabadiliko ya kipengele namba 101 cha katiba, ambacho kinamdhibiti rais kuhudumu kwa miaka miwili, kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Rwanda.

0 comments:

Post a Comment