Takaribani askari 500 wa
Jeshi la Marekani walijiua mwaka jana, na hivyo kuendeleza mkondo wa
idadi
kubwa ya wanajeshi wanaojiua nchini humo katika kipindi cha miaka saba
iliyopita.
Wizara ya Ulinzi ya
Marekani Pentagon katika ripoti yake ya Ijumaa ilisema kuwa, askari 265 walio
katika vikosi vya anga, bahari, nchi kavu na kikosi cha marine walijiua mwaka
2015.
Aidha askari 210 wa
ziada katika jeshi la Marekani walijiua mwaka jana.
Mwaka 2001 wanajeshi 145
walijiua katika Jeshi la Marekani na idadi hiyo imekuwa ikiongezeka kila mwaka.
Msemaji wa Pentagon
Luteni Kanali Hermes Gabrielle, amesema kuzuia vitendo vya wanajeshi kujiua ni
suala linalopewa kipaumbele na Jeshi la Marekani.
0 comments:
Post a Comment