Hatua ya mwanamke mmoja msomi ya kuvua nguo nchini Uganda, imezua mjadala
mkali nchini humo.
Baada ya kukerwa na hatua ya
kufungiwa nje ya ofisi yake na usimamizi wa chuo kikuu cha Makerere, Stella
Nyanzi alivua nguo zote kama njia ya kupinga.
Hata hivyo mwishowe aliruhusiwa
kuingia ofisini mwake,na wengi wa wafuasi wake wanasema kuwa alilazimishwa
kufanya hivyo kutoka na yale aliyokuwa akitendewa.
Hata hivyo wale wanaomkosoa
wanasema kuwa, amekiuka maadili na kwamba mwanamke hastahili kuwa mtupu hadharani.
Gazeti la the New Vision
nchini humo linasema kuwa, waziri anayehusika na maadili anataka Nyanzi
akamatwe.
0 comments:
Post a Comment